• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

BIASHARA ZA MIPAKANI KATI YA TANZANIA NA MSUMBIJI KUIMARIKA

Posted on: February 27th, 2025

Biashara za mipakani kati ya nchi ya Tanzania na Msumbiji zinaenda kuimarika, hii ni kufuatia mabalozi wa nchi hizi mbili kufanya mazungumzo ya kuimarisha usalama, uchumi na mahusiano wa nchi hizi.

Mazungumzo hayo yaliyoitishwa na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Sawala, yamefanyika mapema leo tarehe 27 Februari 2025 yakiwajumuisha Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania ikiwa ni hatua ya awali kabla ya kikao cha Ujirani mwema.

Wengine walioshiriki kikao hiko ni Mkuu wa wilaya ya Mtwara Mhe. Abdallah Mwaipaya, maafisa kutoka Wizara ya mambo ya nje, Wizara ya Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Kamati ya Usalama mkoa wa Mtwara.

“Nia ya kikao hiki ni kujadiliana namna ya kuimarisha mahusiano ya nchi hizi mbili hususan shughuli za kiuchumi na kiusalama lakini hasa tutapanga siku ya kuwa na kikao cha ujirani mwema.” Alieleza Kanali Sawala

Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji ameeleza mahusiano ya kihistoria baina ya nchi hizo mbili hasa wakati wa harakati za kutafuta uhuru wa nchi ya Msumbiji ambapo Tanzania ilishiriki kuwasaidia jambo lililofanya ziwe na mahusiano mazuri mpaka sasa.

“Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inasisitiza kuimarishwa kwa shughuli za kiuchumi. Jukwaa la ujirani mwema litakuwa ni fursa la kuwezesha nchi hizi kutangaza fursa zake na kuimarisha uchumi wa nchi hizi. Mikoa ya jirani yaani Mtwara na Ruvuma kwa upande wa Tanzania na Cabo Delgado na Niassa nchini Msumbiji mashirikiano yao yatafanikisha maendeleo ya utekelezaji diplomasia ya uchumi.” Alieleza Mhe. Phaustine Kasike, Baloziwa Tanzania Nchini Msumbiji.

Nae Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania, Mhe. Ricardo Mtumbaida amepongeza juhudi zinazofanyika kuzidi kuunganisha nchi hizo kiuchumi na kijamii.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • CSR YAIGUSA JESHI LA POLISI NA UHAMIAJI MTWARA

    April 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASHWA KIBAHA; KUKIMBIZWA MIKOA 31.

    April 02, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA MKONO WA EID NA PASAKA MTWARA

    March 31, 2025
  • RC SAWALA AMUAPISHA DC MASASI; AMPA MAELEKEZO

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.