• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

KANALI AHMED ABBAS AHMED AWAONYA BAADHI YA WAFANYABIASHARA WANAOHUJUMU ZOEZI LA USAFIRISHAJI WA KOROSHO KUPITIA BANDARI YA MTWARA.

Posted on: November 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewaonya baadhi ya wafanyabiashara wanaohujumu zoezi la Usafirishaji wa Korosho kupitia bandari ya Mtwara ambapo, amesema kuna viashiria vya hujuma zinazofanywa na watu wenye nia mbaya ya kukwamisha jitihada za Serikali za kukuza pato la Mkoa kupitia zao la Korosho.


Kanali Abbas ametoa kauli hiyo katika ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya leo mchana katika bandari ya Mtwara ambapo ameshuhudia msururu wa malori yaliyokua yakisubiri kuingia ndani kupakua korosho na hivyo kulazimika kutoa maagizo kwa wasimamizi wa kampuni za Usafirishaji.

"Ndugu zangu nimeingia ndani, nimetembelea kila eneo hakuna shida, nimekagua makasha nimejionea yapo ya kutosha yanasubiri mzigo uingie upakiwe, ninachotaka kufahamu ni kwa nini ndani hakuna lori linaloshusha mzigo, lakini hapa nje kuna foleni ya aina hii" Alihoji kwa mshangao Kanali Abbas.

Akizungumza kwa Masikitiko Kanali Abbas aliwaeleza wadau wa Usafirishaji waliokuwa wakisubiri kuteremsha mizigo yao kuwa, tayari Serikali imebaini kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakila njama kuhujumu zoezi hilo na kuonya kuwa Serikali ya Mkoa Itachukua hatua kwa yeyote atakayebainika.


“Kuanzia sasa naagiza, Magari yote yaliyoko hapa nje kwenye foleni yaingie ndani mara moja yaanze kushusha mzigo kama kuna mtu anataka kusafirisha Korosho kwa njia ya barabara alete maombi tutayatathimini kama yana mashiko tutaruhusu, hatutaruhusu figisu figisu katika suala kama hili lenye maslahi makubwa kwa Taifa letu” Alisisitiza Kanali Ahmed Abbas Ahmed.


Zoezi la Kusafirisha Korosho kupitia bandari ya Mtwara ni Utekelezaji wa agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Wakati wa ziara yake ya Mwezi Septemba, 2023 Mkoani hapa, ambapo alisema Serikali inataka Kuona kila mwananchi ananufaika na mnyororo wa thamani katika zao la Korosho.


Aidha mpaka Kufikia Novemba 7, 2023 Jumla ya makasha 335 sawa na tani 8,275.22 zilikuwa tayari zimeandaliwa bandarini hapo zikisubiri kusafirishwa katika nchi Mbalimbali duniani.

Novemba 8, 2023

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.