Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Gasper Byakanwa,
Jana Oktoba, 26 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko katika safu ya Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na Wakuu wa Mikoa kwa kuteua, kupandisha vyeo na kuhamisha vituo vya kazi.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi Ikulu Jijini Dar es Salaam jana imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Mhe. Gelasius Gasper Byakanwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, nafasi ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Mhe. Halima Dendego.
Vilevile Mheshimiwa Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mheshimiwa Joackim Wangabo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
Akizunugmzia mabadiliko hayo, Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego ameandika kwa kifupi kwenye mtandao wa Whatsap unaowahusisha viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa mkoani Mtwara (LGA Leaders);
Ninayo furaha kuona ninaondoka ukiwa salama na nimezalisha RC Mwingine. Hongera sana kaka yangu Wangago Mungu akusimamie. Wadau muendelee kuchapa kazi kwa mwendo uleule Mtwara inazidi kung’aa.
Nitazidi kuwaombea na ninawashukuru kwa ushirikiano mulionipa.
Kwa upande wake Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Evaristy Masuha anasema Mkoa umepokea mabadiliko hayo kwa mikono miwili. Wanaamini mabadiliko haya, bado yana nafasi kubwa kwa Mheshimiwa Dendego kuendelea kulitumikia taifa hili kwa nafasi nyingine. Pia ni nafasi nzuri kwa Mheshimiwa Byakanwa kuendelea kuonesha uwezo wake mkubwa aliouonesha katika kusukuma maendeleo ya wananchi akiwa Wilayani Hai
KARIBU SANA MHESHIMIWA BYAKANWA. KWA HERI MHESHIMIWA DENDEGO.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara
Anuani ya Posta: 544, MTWARA
Simu: +255 23 2333014
Mobile: +255 23 2333014
Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz
Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.