• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

KIKAO CHA KUJADILI CHANGAMOTO NA MIKAKATI YA KUONGEZA IDADI YA KAYA ZINAZOTUMIA CHUMVI YENYE MADINI JOTO YA KUTOSHA MKOANI MTWARA

Posted on: July 4th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara CPA Bahati I. Geuzye, aliongoza kikao cha wadau wa chumvi wa Mkoa wa Mtwara. Kikao hicho kilikuwa na  lengo la kujadili changamoto zinazo kwamisha ongezeko la kaya zinazotumia chumvi yenye madini joto ya kutosha katika Mkoa huo na kuweka mikakati ya pamoja. Alifafanua kuwa, agizo la uandaaji wa kikao hicho lilitolewa na Mhe. Kanali Patrick K. Sawala Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kilichofanyika tarehe 03/05/2024. 


Aliendelea kueleza kwamba, kaya zinazotumia chumvi yenye madini joto ni asilimia 47 na lengo lililowekwa ni asilimia 90 au zaidi. Changamoto zilizobainishwa kukwamisha ongezeko la kaya zinazotumia chumvi yenye madini joto ya kutosha ni ukosefu wa umeme ya kuendeshea mitambo, uhaba wa masoko, madini joto kuuzwa bei ghali, teknolojia duni ya kuchanganya madini joto kwenye chumvi na uhaba wa barabara za kusafirishia chumvi. 


Mkurugenzi Mtendaji kutoka Shirika la Madini la Taifa Bwana Venance B. Mwasse alieleza kuwa, Serikali imepanga kujenga Kiwanda cha chumvi Mkoani Lindi kwenye Halmashauri ya Wilaya Kilwa. Alieleza kwamba, kiwanda hicho kitasaidia Mikoa ya Kusini ambayo ni Lindi na Mtwara kadhalika kitaboresha teknolojia ya uzalishaji wa chumvi kadhalika na kuboresha masoko ya chumvi kwenye Mikoa hiyo. Katibu Tawala wa Mkoa CPA Bahati I. Geuzye alimwelekeza Meneja wa TANESCO Mtwara kuhakikisha wanaandaa kwa haraka mpango wa upatikanaji wa umeme kwenye mashamba ya chumvi ili kuboresha uzalishaji wa chumvi. Aidha, aliwataka wataalamu kuhakikisha wanaimarisha usimamizi na kuwajengea uwezo wazalishaji chumvi ili kuimarisha utaalamu kwenye uchanganyaji wa madini  joto na chumvi.  


Washiriki wengine wa kikao hicho walikuwa ni Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakurugenzi Watendaji kutoka Halmashauri ya Wilaya Mtwara na Manispaa ya Mtwara Mikindani, Meneja TBS Kanda ya Kusini, Kamishna wa Madini Kanda ya Kusini, Mkurugenzi Mtendaji kutoka Neel Salt Limited, Meneja SIDO Mtwara, Meneja TANESCO Mtwara, Mwenyekiti kutoka Chama cha Wazalishaji Chumvi Taifa, Wazalishaji wa chumvi kutoka Halmashauri ya Wiaya Mtwara, Maafisa Lishe, Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Afya ngazi ya Mkoa na Halmashauri.

Kikao hicho kilifanyika kwenye Ukumbi wa Boma, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara.


Julai 4, 2024



Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.