• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Majeshi yasaidie kutoa maarifa ya uzalishaji kwa jamii inayowazunguka

Posted on: August 1st, 2017

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George Simbachawene (wa tatu kutoka Kulia) akiangalia mradi wa uzalishaji wa Samaki katika banda la maonesho la Suma JKT


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George Simbachawene ameyataka majeshi yote nchini kusambaza maarifa ya kilimo bora kwa jamii inayowazunguka. amesema huu ni muda muafaka kwani taifa linapopanga kupiga hatua kuelekea Uchumi wa viwanda ni budi kuhakikisha jamii nzima inashirikishwa kwa kupata maarifa ya teknolojia mpya.

Mheshimiwa Simbachawene ameyasema hayo wakati akifungua maonesho ya Nanenane Kitaifa yaliyofanyika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi leo. Amesema taifa linapokuwa halipo vitani, inatarajiwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania kuwekeza katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali na hata kuisadia jamii kufikia malengo. Badala ya hali kuwa hivyo badala yake imekuwa ni jambo la kawaida kwa maeneo ya Jeshi kuwa na uzalishaji wenye tija kwa mazao ya aina mbalimbali lakini jamii inayowazunguka ikiwa duni.

Amesema jambo hili halikubaliki na kwamba jeshi la wananchi linatakuwa kuwa rafiki wa jamii inayowazunguka. Liweke miundmombinu na mkakati imara wa kuhakiksiha jamii inaiga na kuzalisha kama wao wanavyozalsiha na kwamba hilo si suala la kusubiri jamii iwafuate bali mipango ya jeshi ielekeze huko.

Mheshimiwa Simbachawene ambaye aliridhishwa na ubora wa mabanda ya maonesho ya jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) kwa jinsi walivyopiga hatua kubwa katika uzalishaji amesema hilo ni jambo la kujivunia na kwamba haya yote yanatokana na nidhamu kubwa ya na uamuzi wa dhati wa kuwekeza katika masuala hayo lakini haikubaliki katika jamii iwapo uwezo huo unaishia kwa jeshi tu wakati jamii inayozunguka wanaishi kwa shida na hawana maarifa yoyote ya uzalishaji.

Awali akielezea uzalishaji uliowekezwa na jeshi hilo, Luteni kanali Peter Lushika wa Suma JKT amesema Jeshi limejipanga na limekuwa likitengeneza bidhaa mbalimbali zikiwemo nguo, viatu na mazao ya kilimo. Pia limekuwa likitoa mafunzo mbalimbali ya uzalishaji bora kwa vijana.  

Ametoa wito kwa aserikali kuendelea na msisitizo wa kuwataka wananchi wa Tanzania kutumia na kupenda bidhaa za ndani ili kuinua wazalishaji wa ndani.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego amesema Jeshi la wananchi wa Tanzania Limejipanga lakini bado linapaswa kuhakikisha jamii inaondoa woga wa kupata maarifa kutoka kwa maaskari. Amesema zama za wananchi kuogopa maaskari zimekwisha hivyo jeshi lijipange lihakikishe liko karibu na wananchi. Liweke mazingira ambayo yatawafanya wananchi wawe huru kujifunza kutoka jeshini na hivyo kuwa na mabadiliko ya pamoja kimaendeleo.

Maonesho ya Wakulima Kitaifa maarufu kama Nanenane yamefunguliwa Leo katika viwanja vya Ngongo vilivyoko katika halmashauri ya Manispaa ya Lindi mkoani Lindi. KauliMbiu ya maonesho hayo mwaka huu ni “Zalisha kwa tija mazao ya Bidhaa za Kilimo, Mifugo na Uvuvi ili kufikia uchumi wa Kati.

Maonesho haya ya siku nane yanatarajiwa kufungwa Agosti nane ambapo Mgeni Rasmi natarajwia kuwa Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.