• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MELI YA KWANZA YENYE SHEHENA YA KOROSHO YAANZA SAFARI KUTOKA BANDARI YA MTWARA

Posted on: November 9th, 2023

Mkuu wa mkoa wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema serikali ya Mkoa haitokubali visingizio vya aina yeyote vinavyolenga kudhoofisha jitihada za serikali za kusafirisha korosho nje ya nchi kupitia bandari ya Mtwara.


Kanali Abbas ametoa kauli hiyo mbele ya Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack aliyefika mkoani Mtwara kujionea namna zoezi la usafirishaji wa korosho kupitia bandari linavyotekelezwa.


Katika ziara hiyo Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewaeleza viongozi kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara kuwa mkoa wa Mtwara umesimamia kikamilifu utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa asilimia mia moja na kuongeza kuwa kupitia zoezi hilo mamia ya wananchi wamenufaika kiuchumi.

Akizungumza mara baada ya kukagua zoezi la kuteremsha makasha matupu na kupakia makasha yenye shehena ya korosho kwenye meli inayojulikana kama CMA CGM KAILAS Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amesema wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa vinara wa kutoa taarifa zenye utata ambazo zimechangia kupunguza kasi ya utekelezaji wa zoezi hilo.


“Mhe. Mkuu wa Mkoa, binafsi nimekua nikipata malalamiko kutoka kwa baadhi ya wadau kuhusu suala la miundombinu katika bandari ya Mtwara, wengine wamenilalamikia kuhusu uhaba wa makontena, weninge wanasema eti hakuna meli za kutosha na wengine wameenda mbali zaidi wakasema kuna foleni kubwa sana” alisema kwa mshangao Mhe. Telack.


“Ndugu zangu baada ya ziara yangu bandarini hapa nimebaini kuwa kauli zote zilizotolewa na watu hao ni visingizio vinavyolenga kuupotosha umma kuwa zoezi hili limekosa Ufanisi” aliongeza Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack.


Aidha Mhe. Telack akiwa bandarini hapo ameweza kujionea makasha tupu 1800 yakisubiri kupakiwa korosho ambapo ametoa wito kwa wafanyabiashara na wasafirishaji wenye nia ya kusafirisha mizigo yao kupitia bandari ya Mtwara kufuata utaratibu badala ya kutengeneza visingizio ambavyo vina lenga kuishawishi mamlaka kuruhusu usafirishaji wa korosho kwa njia ya Barabara.


Kwa upande wake meneja wa bandari ya Mtwara Fredinand Nyathi amewahakikishia  wakuu wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuwa bandari ina miundombinu rafiki na ya kisasa inayoruhusu zoezi la kupakia na kupakua mizigo kufanyika kwa muda mfupi.

Aidha Nyathi ameongeza kuwa hivi karibuni bandari ya Mtwara inatarajia kupokea meli zaidi ya 5 zitakazoleta makasha tupu na kuchukua makasha yenye shehena  ya korosho huku kampuni za PIL, CMA na MSC zikiwa tayari zimethibitisha kuleta Meli zake katika bandari ya Mtwara.

Hali-kadhalika Nyathi  amewaomba wakuu hao wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuendelea kuwahamashisha wafanyabiashara na wasafirishaji kuitumia bandari hiyo kama njia kuu ya usafirishaji wa mizigo ya Korosho na bidhaa nyingine.

Katika ziara hiyo pia wakuu wa Mikoa ya Lindi na Mtwara waliishuhudia meli ya kwanza inayojulikana  kama CMA CGM KAILAS ikikamilisha zoezi la kupakia makasha 51 ya korosho baada ya kuteremsha makasha tupu katika bandari hiyo ikiwa tayari kuanza safari kuelekea nje ya nchi.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • CSR YAIGUSA JESHI LA POLISI NA UHAMIAJI MTWARA

    April 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASHWA KIBAHA; KUKIMBIZWA MIKOA 31.

    April 02, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA MKONO WA EID NA PASAKA MTWARA

    March 31, 2025
  • RC SAWALA AMUAPISHA DC MASASI; AMPA MAELEKEZO

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.