• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mtwara RS hoi kwa Polisi shindano la kujaza maji (water relay)

Posted on: December 31st, 2018

Timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara imeshindwa vibaya na Timu ya jeshi la Polisi Mtwara katika mashindanio ya kujaza maji kwenye ndoo.

Mashindano hayo yaliyofanyika wakati wa Tamasha la “Msangamkuu Beach Festival “2018 timu ya Sekretarieti ya Mkoa ilipata nafasi hiyo baada ya shabiki wake Mkuu  Benaya kapinga (Katibu Tawala wilaya ya Tandahimba), kucheza faulo.

Shindano hilo lililokuwa likiwataka washiriki kujaza maji kwenye ndoo ndogo kwa kupokezana mgongoni lilianza kwa mbwembwe huku mchezaji namba moja wa timu ya Sekretarieti ya Mkoa Mhe. Gelasius Byakanwa  (RC) akionesha umahiri katika mbio za kuyafuata maji baharini. Hata hivyo mchezaji huyo alionesha udhaifu wa kumpasia mchezaji aliyekuwa mgongoni kwake Dkt.Jilly Maleko (RAS) hali iliyosababisha maji mengi kuishia mgongoni kwake.

Mchezaji pekee aliyeonekana kuimudu vema nafasi yake katika shindano hili ambalo lilikuwa likifanyika kwa mara ya kwanza mkoani hapa ni Mhe.Evod Mmanda (Mkuu wa Wilaya ya Mtwara), ambaye alionekana kuwa mwepesi kumwaga maji na kukimbia kuchota mengine.

Dalili za kushindwa kwa timu ya sekretarieti zilianza kuonekana mapema baada ya kuanza kuingiza wachezaji kinyemela ambapo Mhe. Sebastian Walyuba (Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba) kuvamia mchezo huo bila taarifa ya refa.

Baada ya kuonekana jahazi la timu ya sekretarieti ya Mkoa linaelekea kuzama ndipo mtumishi wa Sekretarieti ya mkoa Benaya kapinga alijipenyeza katikati ya benchi la ufundi akiwa ameficha maji yaliyokuwa kwenye chupa ya maji ya Kilimanjaro.

Hata hivyo Refa alishtukia ujanja huo wakati mchezaji huyo akiongeza maji hayo kwenye ndoo iliyokuwa imeshikiliwa na Dkt Jilly Maleko(Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara).

Pamoja na jitihada hizo bado ndoo ya timu ya Polisi ilikuwa imeshajaa hali ambayo ilimfanya refa apulize kipenga cha kumaliza mchezo na kumpa nafasi Mkuu wa Mkoa amtangaze mshindi.

Akizungumzia hali hiyo Kapinga amemlalamikia refa kwamba hakuwa makini kwani yeye aliamua kufanya hivyo baada ya kuona wapinzani wao wakifanya hivyo.

“Mimi nimewaona wenzangu wanafanya hivyo hivyo na mimi nikaamua kujibu mapigo. bahati mbaya mimi wameniona lakini mwenzangu hakuonekana”. alisema kapinga.

Kwa upande wake Kocha wa timu ya Sekretarieti ya Mkoa Aziza Mangosongo (Mkuu wa Wilaya ya Newala), ameshukuru kikosi chake na kwamba wanaenda kujiandaa kwa ajili ya tamasha la aina hii ambalo limeonekana kuwavutia wengi.

Aidha, Mhe.Mangosongo amemtetea shabiki wake kwamba mchezo ni mbinu, bahati mbaya mbinu yao imeshtukiwa wakati wenzao wakifanikiwa.

Tamasha la “Msangamkuu Beach festival”limefanyika huku likishuhudiwa na umati mkubwa wa wananchi. Tamasha hilo ambalo limefanyika kwa mara ya kwanza limejumuisha michezo mbalimbali ikiwemo Beach soka, michezo ya watoto, mieleka, kuimba. kucheza, kuogelea na kupiga kasia na mingine mingi.

Video yake hii HAPA

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.