• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mtwara tayari kukabiliana na CORONA

Posted on: March 27th, 2020

Mkoa wa Mtwara uko tayari kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19. Baadhi ya mambo muhimu yaliyozingatiwa katika maandalizi ni pamoja na kutoa elimu sahihi juu ya ugonjwa huo, Kukamilisha mapema Maandalizi ya vifaa muhimu kwa ajili ya kuchukulia sampuli za wagonjwa (tripple packages & VTM), Kutambua maeneo muhimu ambako wahisiwa wa ugonjwa huo watafikishwa, kuwaandaa wataalamu wa maabara. Pia vifaa tiba na dawa muhimu kwa ajili ya kutibu mgonjwa wa aina hiyo vipo.

 Hayo yamebainishwa leo Machi 27 na Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mratibu wa Maabara Mkoa, Edward Ngonyani katika kikao maalumu kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Gelasius Byakanwa kwa ajili ya kupeana elimu maalumu juu ya ugonjwa huo.

Amesema elimu ambayo imekuwa ikitolewa ni pamoja na jinsi ya kujikinga na ugonjwa huo, dalili zake pamoja na hatua za kuchukua inapobainika kuwa na dalili za ugonjwa. Aidha mkoa umetenga vituo vitano kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa watakaobainika kuwa na ugonwa wa COVID-19. Vituo hivyo ni Kituo cha Afya Kilambo ambacho kiko wilaya ya Mtwara, Mkunya ambacho kiko Newala, Mtambaswala kiko Nanyumbu, Mbonde ambacho kiko Masasi pamoja na Majengo.

Naye Afisa Afya Mkoa Sasita Shabani amewataka wananchi wa Mkoa wa Mtwara kuchukua tahadhali hasa kutokana na jiografia ya mkoa Mtwara ambao unapakana na nchi ya msumbiji ambayo pia imegundulika kuwa na wagonjwa wa aina hiyo. Amesema ugonjwa huo unasambaa kwa kasi iwapo tahadhali haitachukuliwa. Amewataka kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola inapobainikika kuwepo na mgonjwa mwenye dalili hizo huku akisisitiza wananchi wasitowe taarifa ambazo hazijapitishwa na mamlaka za serikali na wataalamu wa afya.  

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa Mhe. Gelasius Byakanwa akasisitiza utoaji wa taarifa sahihi ambazo haziwatii hofu wananchi. Amesema hatua zilizochukuliwa na serikali ya Tanzania katika kupambana na ugonjwa huu ni sahihi hivyo zinapaswa kufuatwa.  Amewataka wananchi waendelee na shughuli zao huku wakizingatia taratibu za afya.

Kikao hiki kimefanyika Ukumbi wa Chuo cha Uganga (COTC) kikiwahusisha Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa, Waganga Wakuu wa Wilaya, wakuu wa Taasisi za serikali na Binafsi pamoja na viongozi wa Dini ikiwa ni mwendelezo wa vikao vyenye lengo la kutoa elimu juu ya ugonjwa wa COVID-19 ulioanzia nchini China mwishoni mwa mwaka jana.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.