• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mtwara waomba nyumba ya Nyerere Mikindani ikarabatiwe

Posted on: October 13th, 2018

Kuelekea miaka 19 bila Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere wakazi wa Mtwara Mikindani wameiomba serikali kukarabati nyumba aliyofikia mwalimu Nyerere wakati wa harakati za mapambano ya uhuru. Nyumba hiyo iliyojengwa na Mahajub Mahamoud mmoja wa wanajeshi wa jeshi la Mkoloni imekuwa gofu na kuta zake zimeanza kudondoka.

Akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii wakati wa uzinduzi wa Mji Mkongwe wa Mikindani mapema mwezi huu Mzee Mohamed Kidume ambaye ni moja ya wazee maarufu mjini Mikindani amesema kwa wakati huo nyumba hiyo iliyoko ndani ya hifadhi ya mji Mkongwe wa Mikindani ndiyo nyumba iliyoonekana kuwa na hadhi ya kulala mgeni maarufu kama mpigania uhuru wa Tanganyika mwalimu Julius kambarage Nyerere. Pamoja na umaarufu huo nyumba hiyo imetekelezwa na sasa inaelekea kuanguka.

“Jambo ninalosikitika ni kwamba chama hakitaki kutengeneza hii nyumba, na serikali haitaki kusaidia vilevile. Leo umekuja umekuta zile kuta. Atakapokuja mtu mwingine atakuta huo ukuta haupo. Tafadhali nyumba inakufa na tutakuwa hatuna faida yoyote. Amesema Mzee Kidume”.

kwa upande wake Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Japhet Hasunga amepokea ushauri huo na kumuagiza katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Aloyce Nzuki kuhakikisha nyumba hiyo inakarabatiwa na kukamilika ndani ya mwaka mmoja.

“…na nyinyi kama Wizara ile ya Mwalimu muisimamie. Nawapa mwaka mmoja mhakikishe mmeikarabati yote na imekamilika”.

Akilezea historia ya ujenzi wa Nyumba hiyo Mzee Kidume amesema ilijengwa na Mtanzania aliyejulikana kwa jina la Mahamoud ambaye alikuwa askari wa jeshi la mkoloni makazi yake yakiwa Dar es Salaam.

Aidha ujenzi huo ulikuwa ukisimamiwa na kaka yake aliyejulika kwa jina la Ahmed Adam wakati huo Mahamoud akituma fedha kutokea Ujerumani alikokuwa vitani.

hata hivyo Mahamoud hakuweza kuiona nyumba hiyo kwani alifariki akiwa vitani.


Video yake hii HAPA

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.