• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mtwara watakiwa kupanda miti

Posted on: May 15th, 2017

Kiongozo wa Mbio za Mwenge kitaifa Amour Hamad Amour, amewataka wananchi mkoani Mtwara kupanda miti ili kuhifadhi mazingira. Amour ameyasema hayo leo Wakati akizindua mradi wa shamba la miti la mjasiliamali Joseph Kamkumba lililoko kijiji cha Mchemo Wilayani Newala.

Amesema miti ina umuhimu mkubwa katika kutunza na kuhifadhi mazingira na kuyafanya yaendelee kuwa katika uhalisia. Bila kufanya hivyo mazingira yatapoteza uhalisia na kuchochea majanga mbalimbali yakiwemo majanga ya ukame.

Katika kusisitiza suala hilo amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Newala Mheshimiwa Azizi Mangosongo kuhakikisha anasimamia zoezi hilo na kulifanya shamba la miti la Kamkumba kuwa shamba darasa.

‘Miti ina umuhimu mkubwa katika maisha ya binadamu kwani inasaidia kuzuia upepo ambao ungeweza kuleta madhara katika makazi ya watu. Pia inatunza mazingira na kuyaweka katika uhalisia’. Amesema.

Amour ambaye anaendelea na mbio za Mwenge Mkoani Mtwara kwa siku ya Nne sasa ametoa pongezi kubwa kwa viongozi wa Wilaya na Halmashauri Wilaya ya Newala na kuwataka waendelee na usimamizi wa masuala ya kilimo ili wasaidie wananchi kuyafikia malengo yao.

Kwa upande wake Afisa Maliasili wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Magreth Likonda amesema shamba hilo lenye ukubwa wa ekari 17, miti 5,000 lilianzishwa mwaka 2011 baada ya kupata ushauri kutoka halmashauri.

Baada ya kuanzisha shamba hilo ambalo amekuwa akilipanua kila mwaka limeonesha manufaa ambapo mwaka 2013 Mwenge wa uhuru ulitembelea shamba, likakaguliwa na kupanda miti.

Likonda ameyataja manufaa ya mradi huo kuwa ni pamoja na kuhifadi mazingira, na kukabiliana na upungufu wa mazao ya misitu. Pia kutengeneza ajira kwa wakazi wa eneo hilo. Aidha shamba hilo pia linatumika kama amana kwa kukopa mikopo Benki.

Kwa upande wake mmiliki wa shamba hilo, Joseph Kamkumba  ameshukuru Mwenge wa uhuru kukagua shamba hilo na kuahidi kuongeza jitihada zaidi.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.