• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC amuomba Waziri kuruhusu uzalishaji Pombe ya mabibo

Posted on: April 3rd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa (wa tatu kutoka kulia) akifuatilia jinsi pombe ya mabibo inavyotengenezwa mara alipotembelea wazalishaji wa pombe hiyo katika Kijiji cha Chigugu wilayani Masasi


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa amemuandikia barua Waziri wa Sheria na Katiba kumuomba kufanyiwa marekebisho sheria ya pombe za kienyeji ili iruhusu uzalishaji na utengenezaji wa pombe hizo, huku akimuomba Waziri wa Viwanda kutoa ruhusa kwa wakazi wa Mtwara kuzalisha pombe za kienyeji kwa kutumia mabibo ya korosho.

Akiwasilisha majibu ya Sampuli ya pombe ya mabibo (gongo) iliyotumwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kujua usalama wa kinywaji hicho amesema Mkemia Mkuu amethibitisha kuwa vimiminika hivyo havikukutwa na madini mengine ambayo ni sumu kwa watumiaji.

 “Vimiminika vyote vimekutwa na vileo tofafuti kuanzia 8 mpaka 45.9 na ethano au kilevi salama. Havijakutwa na madini mengine ambayo ni sumu kwa madhara ya watumiaji”. Amesema Byakanwa.

Amesema sampuli hizo zilichukuliwa kwa wazalishaji wa pombe hiyo kutoka katika vijiji vya Chigugu wilayani Masasi ambako alichukua sampuli Nne. Kijiji cha Nambeleketela na Majengo vilivyoko wilayani Mtwara alichukua sampuli saba.

“ … na kwa kuwa pombe hizi zilizopimwa zimekutwa salama na hazina madhara. Nimemwandikia waziri wa sheria na Katiba nikimuomba kufanyiwa marekebisho sharia ya pombe za kienyeji ili sheria iruhusu uzalishaji na utengenezaji wa pombe za kienyeji ikiwa ni hatua ya kukuza viwanda na kuongeza thamani ya bidhaa. …nimemwandikia barua waziri wa viwanda nikimuomba atowe ruhusa kwa wanamtwara kuzalisha pombe za kienyeji kwa kutumia mabibo” 

Byakanwa amesema Mheshimiwa Rais amekuwa mstari wa mbele kusisitiza utafiti na mara ya mwisho akiweka jiwe la Msingi la ujenzi wa barabara ya Mtwara Tandahimba alisisitiza kufanya utafiti wa gongo itokanayo na mabibo ili kubaini kama inafaa kwa matumizi mbalimbali ya binadamu.  Kufuatia agizo hilo Byakanwa aliamua kukutana na wazalishaji wa pombe hiyo ili kupata sampuli ambayo aliiwasilisha kwa mkemia Mkuu wa Serikali.

Aidha amewaagiza wakurugenzi wote wa halmashauri za mkoa huo kuwasajili na kuwatambua watengenezaji wote wa gongo.

“Kwa kuwa mkoa unayo fursa ya nzuri ya kuzalisha bidhaa nyingi zitokanazo na mabibo na zitokanazo na gongo. Ninawaagiza wakurugenzi wote wa halmashauri zote kuwasajili na kuwatambua watengenezaji wote wa gongo wakati tukisubiri maamuzi ya waziri wa viwanda ili tutengeneze kanzi data ya wazalishaji na kiwango cha uzalishaji.”

Mafanikio ya zoezi hili yataongeza thamani ya zao la korosho kutoka kwenye mauzo ya korosho ghafi hatimaye kuongeza mauzo ya mabibo.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.