• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC Mtwara atoa miezi mitatu kila mkazi wa Mtwara kujiandikisha kwenye daftari la wakazi

Posted on: January 20th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe: Gelasius Byakanwa ametoa miezi mitatu kwa wakazi wa Mkoa wa Mtwara  kujiandikisha  kwenye daftari la wakazi lililopo kila Mtaa.

Amesema kuwa kama muda huo utapita na mwananchi hajajiandikisha  hatatoa adhabu yeyote, badala yake mwananchi atakosa huduma mbalimbali kutoka kwenye Ofisi za Serikali ikiwemo barua za utambulisho zinazotakiwa kwenye mabenki na huduma zingine.

Byakanwa amezungumza hayo leo wakati wa uzinduzi wa zoezi la Uandikishaji  kwenye daftari la wakazi kwa Mkoa wa Mtwara lililofanyika kimkoa kwenye Viwanja vya Ofisi ya Kata Shangani  Manispaa Mtwara-Mikindani. Aidha amewataka watendaji kutomkaribisha mgeni yeyote kwenye Mtaa kama hana taarifa za kujiandikisha kwenye mtaa alikotokea.

Amesitiza kuwa ili kuendelea kulinda amani, utulivu  na kuondoa uhalifu  kwenye maeneo yao ni lazima wananchi wakafahamiana kwa kujiandikisha kwenye daftari la wakazi lililoko chini ya Mtendaji wa Mtaa. Pia ameagiza mtu yeyote anapohamia kwenye  mtaa ahakikishe amejiandikisha kwenye daftari hilo ili taarifa zake zingizwe.

Mkuu huyo wa Mkoa amezitaja faida zitokanazo na wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wakazi  kuwa ni pamoja na kusaidia Serikali  kupanga bajeti, mahitaji, na huduma za jamii kwa watu wake kwa kuwa takwimu za idadi ya watu waliopo kwenye mitaa, kata, tarafa, wilaya, mkoa hadi Taifa  zitakuwepo. Faida zingine ni pamoja na kuimarisha Ulinzi na Usalama.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa Mtwara-Mikindani Bi. Beatrice Dominic amesema kuwa Wananchi waliosajiliwa kwenye daftari la wakazi kwa Manispaa ni 46,704 Kati ya Wananchi 115,000 waliokadiriwa kwenye sensa ya  watu na makazi ya 2012. Aidha amesema anatarajia  baada ya uzinduzi huo wananchi watatimiza wajibu wao kwa kujiandikisha kwenye daftari hilo.

Ameongeza kuwa Daftari hilo litatunzwa na Mwenyekiti wa Mtaa husika na kwamba Mwenyekiti atapaswa kujaza fomu kila taarifa mpya zinapojitokeza zikiwemo vizazi, Vifo, kuhama na kuhamia. Aidha Mtendaji wa Mtaa atahakikisha daftari hilo linaingizwa Taarifa, linatunzwa na linatumika ipasavyo.

 Daftari la wakazi lipo kisheria chini ya  sheria ya Serikali za Mitaa Na. 6  ya mwaka 1982, na limechapishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI mwaka 2011.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.