• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC Mtwara atoa saa 48 wauzaji Salfa feki kujisalimisha

Posted on: August 4th, 2017

Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa Mtwara, Aman Lusake akionesha salfa iliyothibitishwa na TPRI kuwa haifai kwa matumizi


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Halima Dendego ametoa saa 48 kwa wote wanaohusika na tuhuma za safirishaji wa Pembejeo zilizoisha muda wake kutoka ghala la Naliendele kwenda wakulima wilayani Tandahimba warejee kujibu tuhuma zinazowakabili.

Amesema pamoja na kwamba suala hilo amelikabidhi kwa Kamanda wa Polisi Mkoa, bado anaagiza wote wanaohusika na tuhuma hizo hata kama wako nje ya mkoa warejee ndani ya saa 48.

Agizo hilo amelitoa leo baada ya uchunguzi uliofanywa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa katika ghala linalotuhumiwa kusafirisha Salfa hiyo kujiridhisha na utata wa ubora wa pembejeo hiyo.

Salfa hiyo inayokisiwa kufikia tani 20 ilisafirishwa kutoka ghala hilo lililoko eneo la Naliendele mkoani Mtwara kuelekea Wialayani Tandahimba na kukamatwa Juni 30 mwaka huu.

Mheshimiwa Dendego amesema ameshatoa maelekezo kwa wakulima wasitumie dawa hiyo na kwamba serikali itaendelea kusimamia kuhakikisha mkulima anapata bidhaa yenye ubora stahili.

Aidha Mheshimiwa Dendego ameeleza kuwa ataunda kikosi kazi kufanya uchunguzi iwapo salfa iliyoenda kwa wakulima ni tani 20 pekee. Uamuzi huo unafuatia taarifa ya wasimamizi wa ghala hilo kwamba walisafirisha tani 20 pekee kati ya tani 75 zilizokuwemo.

Akizungumzia kuhusu tuhuma hizo Mhandisi wa Kilimo Mkoa Amani Lusake amesema Salfa hiyo ilikamatwa mwishoni mwa mwezi wa 6 mwaka huu ikiwa imesafirishwa kwenda Tandahimba na kwamba baada ya taarifa hizo kufikishwa kwa mamlaka ya uchunguzi wa ubora wa salfa hiyo (TPRI) wataalamu hao walitoa taarifa kuwa salfa hiyo imeisha muda wake na kwamba haistahili kwa matumizi.

Kwa upande wake Mkaguzi wa Ndani Bodi ya Korosho Mary Mapunda amesema yeye aliambiwa kuruhusu salfa hiyo kwenda kwa wakulima pasipo kujua iwapo ina ubora stahili. Aidha hata mnunuzi aliyekuja kuichukua alieleza kuwa anaihitaji kwa matumizi ya bustani..


VIdeo ya tukio bonyeza HAPA

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.