• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC Mtwara awataka wadau kukamilisha ahadi ya ujenzi wa madarasa

Posted on: January 30th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa amewataka wadau wa maaendeleo walioahidi kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika halmashauri ya wilaya ya Mtwara kukamilisha ahadi zao.

Hayo ameyasema leo Januari 30, 2019 wakati akipokea hundi ya shilingi milioni 13,258,042 kutoka kwa Meneja mahusiano Shirika la Mendeleo la Petroli Tanzania (TPDC), Marie Mselem kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa shirika.

Amesema TPDC waliahidi na leo wametekeleza ahadi. Ni vema na wengine nao wakakumbuka walichoahidi na kukamilisha.

“Baada ya kuzunguka halmashauri yote ya Wilaya ya Mtwara tuligundua shule kumi zilikuwa na matatizo ya vyumba vya madarasa. tuliitisha kikao cha wadau wa maendeleo. Baadhi wametimiza ahadi zao, wengine hawajatimiza. wako walioahidi fedha na wengine vifaa. Nawaomba wakamilishe kama walivyoahidi mbele ya wadau wenzao”. Amesema Byakanwa

Awali akiwasilisha hali ya ujenzi wa vyumba hivyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, Omari Kipanga amesema katika harambee iliyofanywa na Mhe. Mkuu wa Mkoa mapema mwaka jana zilipatikana fedha na vifaa ambavyo thamani yake ilikuwa shilingi milioni 160. Mahitaji ya jumla zilitakiwa milioni mia sita kukamilsha miundombinu yote.

Milioni 160 zilizopatikana wakati huo zilitumika kunyanyua maboma 48 ambapo 16 kati yake yalikamilika kupauliwa na kuezekwa. Maboma 32 bado yanahitaji fedha ili yakamilishwe.

Amesema kwa upande wa Halmashauri wameshanunua Bando 159 za bati ambazo zinatosheleza kuezeka maboma yote 32. Hivyo bado wanahitaji nguvu ya ziada toka kwa wadau ili kukamilisha hatua nyingine za ujenzi.

Kwa upande wake Menja wa TPDC, Marie Mselem amewashukuru wananchi wa Mtwara kwa ushirikiano wao. Amesema Mtwara ni nyumbani hivyo Shirika linakumbuka kurudisha nyumbani kidogo wanachokipata.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU 2025 KUPOKELEWA MKOANI MTWARA MEI 17

    May 15, 2025
  • MTWARA TUKO TAYARI KUUPOKEA NA KUUKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025

    May 14, 2025
  • UFUTA NA MBAAZI KUPIMWA KIDIGITALI MKULIMA KUPATA RISTI KUPITIA SIMU YAKE

    May 14, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE. KANALI PATRICK SAWA AKAGUA MRADI WA MAENDELEO TANDAHIMBA

    May 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.