• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Serikali yatoa ufafanuzi sakata la korosho

Posted on: June 27th, 2018

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mwanasheria Mkuu wa serikali Dkt. Adelardus Kilangi imetoa ufafanuzi kuhusu sakata la korosho lililotawala kwenye vyombo vya habari hivi majuzi. Sakata hilo liliwahusisha baadhi ya waheshimiwa wabunge ambao walionesha kutoridhishwa na pendekezo la serikali kufuta ushuru wa asilimia 65 wa fedha zinazotokana na mauzo ya korosho nje zilizokuwa zikielekezwa katika mfuko maalumu wa kuendeleza zao la korosho.

Akielezea Leo Bungeni kupitia video inayopatikana kwa Kubonyeza HAPA, Dkt. Kilangi anafafanua kuwa sheria mbalimbali za nchi hazizuii serikali kufanya uamuzi unaokusudiwa. Amezitaja sheria hizo kuwa ni pamoja na  Cashew nut Board of Tanzania Act (1884), Cashew nut Marketing Regulations (1996), Maelekezo ya serikali ya mwaka 1998. Kesi iliyofunguliwa na Mfuko wa Kuendeleza zao la Korosho mwaka 1999, Waraka wa Baraza la Mawaziri Namba 42 wa mwaka 2005, Finance Act (2006), pamoja na ‘Memorandum of Understanding’ ya wadau wa korosho ya mwaka 2010.

Ameendelea kuwa hoja hiyo pia inaweza kupata ufafanuzi zaidi kupitia kesi ya Mfuko wa Kuendeleza zao la Korosho ya mwaka 1998 ambapo serikali ilishtakiwa baada ya kuzuia Bodi ya Korosho kupeleka fedha hizo kwenye mfuko wa kuendeleza zao la korosho. Kesi hiyo namba 2004 iliyofunguliwa mwaka 1999 ilipelekea mfuko kushindwa kesi mahakamani, kisha kushindwa tena baada ya kukata Rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa. Aidha Mahakama ilitoa ufafanuzi kuwa makusanyo hayo ni fedha za umma na kwamba bodi ya korosho inakusanya fedha hizo kwa niaba ya serikali na kwamba serikali ndiyo yenye maamuzi juu ya hizo fedha.

Pamoja na maamuzi ya mahakama ambayo yanaipa nguvu serikali bado utaratibu wa kuundwa kwa Mfuko wa kuendeleza zao la korosho haukuweka sheria ambayo inaizuia serikali kuondoa fedha hizo ambazo sasa inakusudia kuzielekeza hazina.

Anaeleza kuwa mwaka 2010 wadau walianzisha mfuko wa kuendeleza zao la korosho lakini bado Memorundum of Understanding iliyopelekea uamuzi wa kuunda Mfuko huo haikutaja iwapo export Levy itakuwa moja ya vyanzo vyao vya fedha. Aidha mfuko huo haukuanzishwa kwa sheria ya Bunge bali ulianzishwa kama Trust.


Mheshimiwa Mwenyekiti Serikali haiwezi kulipa fedha kwenye mfuko ambao haujaanzishwa kwa sheria iliyotungwa na Bunge’. Anaeleza Dkt Kilangi.  

Sikiliza Vdeo HAPA

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.