• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

SIMAMIENI KIKAMILIFU SEKTA YA ELIMU: KANALI ABBAS

Posted on: January 31st, 2023

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amefanya ziara ya siku moja katika wilaya ya Tandahimba kukagua maendeleo katika sekta ya elimu ili kujiridhisha na takwimu za uandikishaji wa wanafunzi wa kidato cha kwanza.

Katika ziara hiyo Kanali Abbas pia amekagua mradi wa vyumba vine vya madarasa uliogharimu kiasi cha Tsh. Milioni 80 katika shule ya sekondari ya Tandahimba ambapo ameonesha kuridhishwa na utekelezaji wa  mradi huo.

“Ndugu zangu wana Tandahimba vyumba hivi vinne mnavyoviona mbele yenu ni sehemu ya mradi wa vyumba 134 ambavyo Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliutengea mkoa wetu kiasi cha Tsh bilioni 2.6 kutekeleza mradi wa kuboresha miundombinu katika shule zetu za sekondari kama njia ya kuwasaidia wanafunzi wa kidato cha kwanza” alisema Kanali Abbas.

Aidha Kanali Abbas amewataka viongozi wa wilaya pamoja na walimu kuendelea kusimamia ipasavyo sekta ya elimu wilayani humo kama njia ya kusaidia kupata matokeo mazuri ya wanafunzi.

“nichukue fursa hii kuwapongeza sana kwa matokeo mazuri ya kidato cha nne mliyoyapata, bila shaka hii ni ishara nzuri kwa wilaya yenu  kuwa na kiu ya kufanya vizuri zaidi katika siku za usoni” aliongeza Kanali Abbas.

Halikadhalika Kanali Abbas ameitumia fursa hiyo kuwahimiza walimu kusimamia vema suala la utunzaji wa mazingira ya shule hiyo ili yafanane na ubora wa miundombinu yake.

Pia mkuu wa mkoa Kanali Ahmed Abbas Ahmed alikagua ujenzi wa zahanati uliotekelezwa kwa nguvu za wananchi katika kata ya Mnyawi, ambapo aliunga mkono jitihada hizo kwa kukabidhi vifaa vya ujenzi ikiwemo mabati 200 na mifuko 20 ya sementi, vifaa ambavyo ni michango ya viongozi mbalimbali wa wilaya ya Tandahimba.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.