• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Taasisi ya Elimu Watakiwa Kusimamia maudhui ya Uandishi wa vitabu

Posted on: April 28th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda akipokea Vitabu toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Elimu Tannzania Profesa Benadeta Kiliani


Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda ameitaka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kuhakikisha inasimamia maudhui yanayozalishwa katika vitabu ili yalenge matakwa ya jamii ya watanzania. Amesema vitabu vinahifadhi maarifa ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa lolote duniani hivyo usimamizi imara wa maudhui yanayowekwa kwenye vitabu ni muhim kwa maendeleo ya Taifa.

Mheshimiwa Mmanda ameyasema hayo leo wakati akipokea vitabu vilivyotolewa na Tasisi hiyo kwa mkoa wa Mtwara katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Mtwara.

Amesema hana mashaka na kazi ya Taasisi ya Elimu Tanzania kutokana na weledi wanaouonesha katika kusimamia kazi zao hivyo moyo huo unapaswa kuendelea ili kuzalisha taifa la wazalendo.

Akizungumzia juu ya mapokezi ya vitabu hivyo Mheshimiwa Mmanda ameshukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuwa na nia ya dhati ya kulifikisha taifa katika malengo yaliyokusudiwa. Amesema serikali ya awamu ya tano tangu ilipoingia madarakani ililenga kuhakikisha kila mwanafunzi anakuwa na kitabu cha kujifunzia na azima hiyo imefikiwa

Ametoa wito kwa walimu wahakikishe wanavitumia vitabu hivyo badala ya kuvifungua ofisini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Elimu Tanzania, Profesa Benadeta Kiliani amesema zoezi la usambazji wa vitabu Tanzania Bara lilianza mwezi Februali mwaka huu na limekuwa likienda vizuri.

Amezitaka halmashauri zote zilizokwisha pokea vitabu hivyo wavisambaze haraka shuleni hatimaye kwa wanafunzi ambao ndio walengwa.

Amevitaja vitabu vinavyosambazwa kuwa ni vitabu vya kiada kuanzia darasa la kwanza hadi la Nne. Pia kiongozi cha Mwalim. Hadi Februali 27 mwaka huu walikuwa wamesambaza vitabu vya darasa la kwanza hadi la tatu kwa mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Tanga, Dodoma, Singida, Manyara Arusha na Mwanza. Aidha kati ya April 29 hadi Mei 5 mwaka huu watakuwa wameifikia mikoa ya  Simiyu, Shinyanga, Pwani na Mara.

Akizunguza kwa niaba ya Maafisa Elimu Mkoa wa Mtwara, Afisa Elimu Msingi, Halmashauri ya Mji wa Nanyamba, Said Farahani amesema uamuzi wa serikali kusambaza vitabu hivyo ni mzuri. Amesema hiyo ndiyo njia sahihi ya kulifikisha taifa katika maendeleo yaliyokusudiwa.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.