• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

VIJIJI VYOTE 785 MKOANI MTWARA VYAUNGANISHWA NA UMEME WA REA.

Posted on: September 9th, 2024

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Kirumbe Ng’enda pamoja na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga Leo tarehe 09/09/2024 wamefanya ziara mkoani Mtwara kwa lengo la kukagua miradi inayotekelezwa na Wizara ya Nishati  pamoja na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

“Pamoja na majukumu mengine, bunge pia lina kazi ya kuishauri na kuisimamia serikali; Leo tumekuja kuangalia na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Wizara kupitia TPDC ikiwa ni pamoja na  gesi. Lakini pia kamati hii inaiagiza Tanesco wafanye matengenezo ya mitambo chakavu.” Alisema Mhe. Ng’enda.

“Hali ya Upatikanaji wa nishati ya umeme baada ya kusimikwa mtambo wenye kuzalisha umeme Megawat 20 unaozalishwa kwa gesi asilia  imekuwa ya kuridhisha kwani wananchi na wawekezaji wanapata umeme wa uhakika.” Alieleza Bw. Patrick Kyaruzi, Mchumi kutoka Ofisi ya Mkoa wa Mtwara.

Aidha, Bw. Patrick aliongeza kueleza kuwa Mkoa wa Mtwara una vijiji 785 ambavyo katika mradi wa REA vijiji vyote vimeweza kuunganishwa Nishati ya umeme.

Miradi iliyotembelewa na kamati hiyo ni pamoja na visima vya uzalishaji gesi vya Mnazi Bay, miradi miwili ya kurudisha fadhila kwa jamii-CSR (Ujenzi wa kituo cha Polisi na Kituo cha Afya) inayotekelezwa na TPDC katika eneo la Msimbati pamoja na mitambo ya kuchakata gesi asilia iliyopo Madimba.


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.