• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Viongozi wa Taasisi za Serikali watakiwa kutozuia utoaji wa taarifa.

Posted on: March 27th, 2017

Viongozi wa Taasisi za Serikali watakiwa kutozuia utoaji wa taarifa.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda amewataka viongozi wa Taasisi za Serikali kutozuia taarifa muhimu kwa wananchi kuingizwa kwenye Tovuti.

Akifunga mafunzo ya siku saba ya uanzishaji wa Tovuti yaliyokuwa yakifanyika katika ukumbi wa Tiffany Diamond Hotel leo, amesema serikali ya Tanzania inasisitiza utawala bora na inaendeshwa kwa uwazi, hivyo suala la kubania taarifa halitavumilika. Amesema Lengo la serikali ni kuwafikia wananchi wote kwa Wakati na ndiyo maana imewaajili Maafisa Habari na TEHAMA ili kuhakikisha lengo hilo linafikiwa.

Mmanda ambaye aliambatana na Kaimu Katibu Tawala Mkoa Elias Nyabusani katika zoezi hilo amewataka Maafisa Habari wasisubiri wananchi waandamane hadi ngazi za juu kwa sababu ya kutopata taarifa sahihi bali wawe chanzo cha kuondoa usumbufu na wingu  la upotoshaji wa taarifa kwa kuweka taarifa sahihi kwa Wakati kwenye tovuti.

Aidha mewataka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhakikisha wanasaidia kusukuma ajira za Maafisa TEHAMA na Maafisa Habari kwani ziko Halmashauri nyingi ambazo hazina wataalamu wa kada hiyo.

Kwa Upande wake Mkuu wa timu ya wawezeshaji, Edgar Mdemu amesema mradi huo unaodhaminiwa na USAID umezindukiwa leo kitaifa mjini Dodoma na kwamba wanatarajia matumizi ya Tovuti yatasaidia kurrahisisha shughuli za serikali na hivyo kusukuma maendeleo ya taifa.

Aidha, Afisa Habari wa Halmashauri ya Manispaaa ya Mtwara Mikindani, Jamad Omari ameshukuru kwa kupata mafunzo hayo na kwamba yamesaidia Manispaa ya Mtwara Mikindani kusukuma maendeleo hasa katika kipindi hiki ambacho wanaweka mazingira ya kuvutia wawekezaji.

Mafunzo ya utengenezaji wa Tovuti yalifunguliwa Machi 20 na kufungwa Machi 27 ambapo kitaifa zoezi la ufungaji limefanyika mjini Dodoma.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MTWARA KUPELEKA TIMU UMITASHUMTA 2025

    June 03, 2025
  • TAASISI YA SPORT DEVELOPMENT AID IMETOA VIFAA VYA MICHEZO KWA WANAFUNZI

    June 02, 2025
  • UNICEF KUSAIDIA WATOTO MTWARA

    June 02, 2025
  • MSIMU WA 3 WA MADAKTARI WA SAMIA; MTWARA YAPOKEA MADAKTARI BINGWA 63

    June 02, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.