• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

WAELIMISHENI WAZAZI UMUHIMU WA KUWEKEZA KATIKA ELIMU - KANALI AHMED ABBAS AHMED; MKUU WA MKOA WA MTWARA.

Posted on: February 13th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewataka Waalimu na Viongozi wa Elimu  waliohitimu mafunzo ya uongozi katika elimu kuitumia elimu waliyoipata kuongeza ufanisi katika sekta ya elimu mkoani humo.

Kanali Abbas ameyasema hayo katika hafla ya kuwatunukia vyeti wahitimu 1014 wa mafunzo hayo iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari Mustapha Sabodo, na kusema kuwa anaamini ujuzi walioupata utachangia kuboresha utendaji kazi wao ikiwa ni pamoja kuwaongezea mbinu na umahiri wa kitaaluma ili kuusaidia  mkoa kufikia malengo yake ya kupandisha kiwango cha ufaulu.

Katika mafunzo hayo yaliyotolewa na Wakala wa Maendeleo ya Elimu (Agency for Develepment of Education Management - ADEM) kwa muda wa wiki tatu yakiwashirikisha Wakuu wa Shule za Awali na Msingi, Sekondari na Maafisa Elimu kata, Kanali Abbas amewataka wahitimu wote kuwa mabalozi pindi watakaporejea katika maeneo yao ya kazi na kusisitiza kuwa anatarajia  wataitekeleza kwa vitendo elimu hiyo na kuitumia kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo.

“Ndugu zangu viongozi leo ninafuraha kubwa ninapokabidhi vyeti hivi kwenu kwani katika matokeo ya Taifa ya mwaka huu 2022/2023 tumepiga hatua kubwa ikilinganishwa na mwaka jana, kwa dhati kabisa nawapongeza katika ngazi zote, Halmashauri, Wilaya na pia Mkoa kwa usimamizi mzuri uliowezesha matokeo haya kupatikana “ alisema Kanali Abbas.

Aidha, kanali Abbas amewataka waalimu waliohitimu mafunzo hayo kujenga mahusiano mazuri kati yao na wazazi ili waweze kuwahamasisha kutambua umuhimu wa kuwapeleka watoto wao shule ili kuongeza kiwango cha udahili mkoani Mtwara.

“Ukiangalia takwimu zinaonesha bado tupo kwenye asilimia 88.17 za uandikishaji, hizo ni takwimu za hivi karibuni nikimaanisha Februari 2023, naomba muongeze bidii kwa kuwahamasisha wazazi wengi zaidi wawaandikishe watoto wao katika shule za msingi na kwa wale waliofaulu kwenda sekondari  wazazi wao wawajibike kuwasimamia” aliongeza kanali Abbas.

Pia Kanali  Abbas, amewakumbusha  waalimu na viongozi wa elimu kuhakikisha huduma ya chakula cha mchana kwa wanafunzi inapewa kipaumbele na kusisitiza kuwa utaratibu huo ndio silaha ya kuongeza ufanisi katika sekta ya elimu na pia kuwashawishi wanafunzi kupenda elimu.

 Aidha Kanali Abbas ameipongeza  ADEM, kwa kukubali kutoa mafunzo hayo na kusema kuwa Serikali ya Mkoa itahakikisha inawasimamia kwa karibu viongozi wote waliohitimu ili waweze kwenda sambamba na malengo ya mafunzo hayo.

Akiwasilisha taarifa ya mafunzo hayo kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Katibu Tawala Msaidizi Rasilimali watu Renatus Mongogwela amesema  Mkoa kwa muda mrefu umekuwa na utamaduni wa kuwajengea uwezo viongozi na wataalamu wake kupitia kozi mbalimbali hatua ambayo imewaongezea weledi wa kutekeleza majukumu yao kikamilifu katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu.

Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wakuu wa shule za Msingi, Sekondari na Maafisa Elimu kata na kuwawezesha kusimamia ufundishaji na ujifunzaji fanisi wenye kuzingatia ujuzi kwa kutumia fursa na uwezo uliopo.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.