• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

WAPENI USHIRIKIANO WAWEKEZAJI KUKUZA UCHUMI: KANALI SAWALA

Posted on: December 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala leo Novemba 29,2024 amefanya ziara katika Kiwanda cha Kuzalisha Simenti cha Dangote kilichopo katika halmashauri ya Wilaya ya Mtwara vijijini ambapo amejionea miundombinu inayotumika katika uzalishaji wa bidhaa hiyo.


Mara baada ya kuwasili kiwandani hapo majira ya mchana Kanali Sawala alipewa taarifa ya mwenendo wa uzalishaji na Kisha akafanya ziara kukagua maeneo mbalimbali ikiwemo eneo linalotumika Kuzalisha malighafi, kituo cha kupokea gesi pamoja na mfumo mzima wa uzalishaji kuanzia Simenti inapotengenezwa mpaka kufikia hatua ya mauzo ambapo aliupongeza uongozi wa Kiwanda Kwa kusimamia vizuri uwekezaji huo.


Halikadhalika ziara hiyo ilimwezesha Kanali Sawala kukutana na madereva wanaosafirisha Simenti kutoka kiwandani hapo kuelekea maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi katika kikao kilichodumu Kwa takribani Saa 1:24 ambapo walipata fursa ya kuwasilisha hoja zao mbele yake.


Miongoni mwa hoja hizo ni pamoja na maslahi duni yasiyoendana uzito wa majukumu yao, kuchelewa Kwa mishahara pamoja urasimu wakati wa kutoa mzigo nje ya kiwanda ambapo wamekuwa wakipewa kauli zinazokinzana kuhusu kufunika mzigo.


Akitoa majibu baada ya kusikiliza pande zote, Kanali Sawala amesema serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki Ili kuhakikisha wawekezaji pamoja na jamii inayozunguka eneo la mradi inanufaika.


"Ndugu zangu madereva bila shaka Kila mmoja wenu ni shuhuda wa faida tunayoipata kupitia Kiwanda hiki ikiwemo ajira, hivyo nawasihi wapeni ushirikiano wa kutosha wawekezaji hawa, jengeni utamaduni wa kutatua changamoto zenu Kwa njia ya Maridhiano sio manung'uniko au migomo" alisema Kanali Sawala.


Kuhusu hoja ya kuchelewa Kwa mishahara ya madereva, Kanali Sawala ameuagiza uongozi wa Kiwanda hicho kuweka utaratibu rafiki utakaohakikisha Kila dereva anapata mshahara wake Kwa wakati ifikapo mwisho wa mwezi.


Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na kamati za usalama za Mkoa na Wilaya, watendaji na viongozi kutoka taasisi za umma pamoja na wataalamu.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU 2025 KUPOKELEWA MKOANI MTWARA MEI 17

    May 15, 2025
  • MTWARA TUKO TAYARI KUUPOKEA NA KUUKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025

    May 14, 2025
  • UFUTA NA MBAAZI KUPIMWA KIDIGITALI MKULIMA KUPATA RISTI KUPITIA SIMU YAKE

    May 14, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE. KANALI PATRICK SAWA AKAGUA MRADI WA MAENDELEO TANDAHIMBA

    May 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.