• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Wengi wajitokeza kupima VVU

Posted on: May 25th, 2017

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Beatrice Dominic akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2017 Mkoani Hapa.


Mbio za Mwenge wa uhuru 2017 zimehitimishwa mkoani hapa juzi na kuacha mengi yenye manufaa. akizungumza Wakati wa kukabidhi Mwenge huo kwa uongozi wa mkoa wa Lindi. Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego amesema moja ya mazuri yaliyoletwa na mwenge wa Uhuru 2017 ni pamoja na hamasa kubwa katika upimaji wa Virusi vya UKIMWI.

Amesema jumla ya wananchi 2284 walijitokeza kupima maambukizi ya virusi vya UKIMWI wakiwemo wanawake 683 na wanaume1661. Waliogundulika kuwa na virusi vya Ukimwi ni 39 wakiwemo wanaume 19 na wanawake 20 sawa na asilimia 1.7. Aidha katika mkesha wa mwenge uliokuwa ukifanyika kila halmashauri, viongozi walihamasisha matumizi ya kondomu ambapo jumla ya kondomu 7236 za kiume zimegawiwa.

 Kwa upande wa uchangiaji damu Dendego amesema wananchi walijitokeza na kuchangia jumla ya unit 135. Aidha suala la mapambano dhidi ya malaria lilipewa msisitizo ambapo wananchi 741 walijitokeza kupima malaria wakiwemo wanaume 509 na wanawake 212.  Waliokutwa na vimelea vya malaria ni 101 wakiwemo wanaume 57 na wanawake 44 sawa na asilimia 5.04.

Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Amour Hamad Amour ameshukuru kwa ushirikiano mzuri walioupata yeye na wenzake kwa kipindi chote cha siku 10 walizokaa mkoani Mtwara.

Amesema yako maagizo mengi waliyoyatoa hapa mkoani na yametekelezwa haraka na kwa Wakati jambo ambalo linampa imani na utendaji mzuri wa viongzoi wa Mkoa wa Mtwara.

Amewataka viongozi wa mkoa kuendeleza umoja huo ili kuendana na falsafa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Joseph Pombe Magufuli ya “Hapa Kazi Tu”.

Mwenge wa Uhuru 2017 uliwasili moani Mtwara tarehe Mei 12 ukitokea mkoani Ruvuma na kukabidhiwa Mkoani Lindi Mei 21.

MWENGE WA UHURU. KARIBU TENA MKOANI MTWARA

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.