• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mtwara waanza kutumia Gesi Asilia Majumbani

Posted on: September 18th, 2019

Waziri wa Nishati Mhe. Medard Kalemani amezindua matumizi ya Gesi Asilia majumbani kwa mkoa wa Mtwara. Mradi huu wa awali kwa mkoa wa Mtwara utagharim shilingi Bilioni 3.7 ambazo ni fedha za ndani za Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Akizindua mradi huo Mhe. Kalemani amesema Awamu ya kwanza ya mradi itazihusisha kata tatu za Reli, Shangani na Likombe zilizoko Manispaa ya Mtwara Mikindani ambapo jumla ya wateja mia tatu watafikiwa. Amesisitiza kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali zao huku ikipunguza uharibifu wa mazingira.

Amesema asilimia 71.25 ya watanzania wanatumia mkaa na kuni ambazo zinapelekea uharibifu wa mazingira.

Kuhusu matumizi ya gesi asilia kwenye magari amesema wako katika mazungumzo na Chuo cha Ufundi Stadi (VETA-Mtwara) kwa lengo la kupata eneo ka kusimika miundombinu ya utoaji wa huduma hiyo. Lengo ni kukamilisha mradi huo ifikapo Desemba mwaka huu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda ameipongeza serikali kwa kuwezesha utekelezaji wa mradi huo. Amesema mkoa wa Mtwara ni moja ya maeneo ambayo yameathirika na ukataji wa miti kwa ajili matumizi ya kuni na Mkaa.

“Kwa asili wilaya na mkoa wetu si eneo lenye miti mikubwa. Ni eneo lenye miti midogo na vichaka kiasi. Ukatataji wa miti kwa ajili ya uchomaji wa Mkaa ulikuwa ukitupeleka kwenye hatari kubwa, Ujio wa Gesi asilia utasaidia kwa kiasi kikubwa kurudisha mazingira katika hali yake.” Amesema Mmanda.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petrol Tanzania(TPDC), James Mataragio amewaondoa mashaka wananchi na watumiaji wa gesi asilia kwamba iko salama sana tofauti na gesi ya mitungi.

“Gesi hii ni salama na zaidi ukilinganisha na gesi ya kitungi (LPG) ama mafuta ya taa au kuni. usalama huu unasabaishwa na tabia yake kwani ni nyepesi kuliko hewa tunayovuta hivyo kupelekea kupotea hewani mapema ikitokea imevuja kwenye jiko kwa namna yoyote na kuondoa uwezekano wa kulipuka na kusababisha moto.”

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MTWARA KUPELEKA TIMU UMITASHUMTA 2025

    June 03, 2025
  • TAASISI YA SPORT DEVELOPMENT AID IMETOA VIFAA VYA MICHEZO KWA WANAFUNZI

    June 02, 2025
  • UNICEF KUSAIDIA WATOTO MTWARA

    June 02, 2025
  • MSIMU WA 3 WA MADAKTARI WA SAMIA; MTWARA YAPOKEA MADAKTARI BINGWA 63

    June 02, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.