• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mwenyekiti CCM aitaka Bodi ya Korosho kuongeza uzalishaji

Posted on: February 20th, 2020

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mtwara Yusufu Nanilla amemtaka Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya korosho Nchini Francis Alfred kutatua changamoto iliyosababisha kushuka uzalishaji wa zao la korosho. Amesema katika miaka ya 1990 uzalishaji wa korosho Mkoani Mtwara ulikuwa mkubwa ukilinganisha na miaka ya hivi karibuni.

Kauli hiyo ameitoa leo katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa wa Mtwara kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu Tawi la Mtwara. Amesema korosho ni zao muhimu na ndiyo maana mikoa mingi imejitokeza kuanza kulima na kwamba kama mkoa wa Mtwara utaendelea kulalamika na kuibua sababu zisizo na msingi, zao hilo litaendelea kushuka.

Awali akiwasilisha taarifa ya zao hilo Mkurugenzi wa Bodi hiyo Francis Alfred alisema uzalishaji wa korosho umeshuka musimu wa 2019/2020 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kukosekana kwa magunia ya kufungashia pamoja na mabadiliko ya Tabia Nchi. Msimu wa mwaka 2019/2020 mkoa ulizalisha tani 132,553 tofauti na uzalishaji wa mwaka 2018/2019 ambapo mkoa ulizalisha tani 124,041.58. hata hivyo ongezeko hilo linakinzana na uzalishaji mkubwa uliokuwa ukifanyika kwa misimu ya mwaka 2017/2018 kurudi nyuma jambo ambalo linamfanya mwenyekiti wa Ccm mkoani Mtwara bwana Nanilla kuhoji ni kwa nini uzalishaji umeshuka hivyo.

Amesema changamoto ya vifungashio inaweza kuwa moja katika changamototo nyingi ambazo zikifanyiwa kazi uzalishaji utapanda.

“Wako wataalamu wengi humu ambao walishiriki kupandisha uzalishaji katika miaka ya 90,  ambapo uzalishaji ulikuwa unafikia zaidi ya tani 190,000. Watumieni hao, mtowe elimu kwa jamii. Hadhi ya zao la korosho itarudi kama kawaida.”

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa ameunga mkono hoja hiyo na kuitaka Bodi ya Korosho kuitisha kikao ili kujadili sababu mbalimbali zinazogusa zao la korosho ikiwemo kutokupanda kwa bei wakati mahitaji ya wanunuzi yalikuwa makubwa. Amesema takwimu za uzalishaji msimu wa 2019/2020 mahitaji ya wanunuzi ilikuwa ni tani 496,667 ikilinganishwa na kiasi kilichozalishwa cha tani 132,553. Aidha, korosho hiyo iliuzwa kati ya shilingi 1400 na 2890.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.