• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Bado tani 2 rekodi ya korosho ivunjwe Mtwara.

Posted on: December 21st, 2017


Rekodi ya uzalishaji wa korosho mkoani Mtwara inaelekea kuvunjwa baada ya uzalishaji kufikia tani 171,000. Akizungumza na mwandihsi wetu, Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji mkoa wa Mtwara Amani Rusake anasema hadi mnada wa 09 uliofanyika Desemba 15, 2017 kwa vyama vyote vya ushirika mkoani hapa, TANECU na MAMCU uzalishaji ulifikia tani 171,000.

Anasema kwa hali ilivyo hana shaka kuwa minada inayofuata, uzalishaji utazidi ule wa mwaka jana. Rekodi ya juu ya uzalishaji wa korosho uliowahi kufikiwa ni msimu wa mwaka jana 2016/2017 ambapo uzalisjhaji ulifikiwa tani 172,681.

Licha ya rekodi ya uzalishaji kuwa juu bado rekodi ya bei ya korosho imeendelea kuvunjwa ambapo kwa musimu huu bei ya juu imefikia shilingi 4055 kwa kilo wakati bei ya chini ikiwa shilingi 3790 Tofauti na rekodi iliyokuwepo ya musimu wa mwaka jana ambapo bei ya juu ilifikia shilingi 4000 kwa kilo wakati bei ya chini ikiwa shilingi 2600.

Wakizunugmzia hali hiyo wananchi wamepongeza serikali ya awamu ya tano kwamba imekuja na muarobaini ambao umesaidia wakulima kuimarisha mashamba yao na hivyo uzalishaji kuongezeka. Wanasema kwa miaka mingi wakulima wa korosho walikuwa wakilalamika serikali kutowajali hali ambayo ilisabisha uzalishaji kupungua.

Katibu wa chama cha Msingi Kusila kijijini Chigweje wilayani Nanyumbu, Sarafina Mohamed anasema sababu kubwa ya ongezeko hili ni kuimarika kwa bei ya korosho hali ambayo imesababisha wakulima kurudi mashambani na kufufua mashamba yaliyokuwa yametelekezwa. Anasema musimu wa mwaka jana aliuza tani 100 lakini mwaka huu hadi mnada wa 08 alikuwa maeuza tani 130. Anasema bado ana matumani ya kupokea korosho zaidi.

Kwa upande wake mkulima maarufu wa korosho kijijini hapo, Lukas Chilonji anasema pamoja na ukweli kwamba kuimarika kwa bei ya korosho ni sababu kubwa ya uzalishaji wa zao hili kuongezeka bado uamuzi wa serikali kuondoa michango mingi iliyokuwa ikiwaumiza wakulima umechangia kwa kiasi kikubwa uzalishaji kuongezeka.

Maboresho yaliyofanywa na serikali ya wamu ya tano ni pamoja na Utoaji wa pembejeo bure kwa wakulima, kuondoa ushuru wa magunia, pia ushuru wa unyaufu. Hali hiyo Imewafanya wakulima ambao walikuwa hawathamini kilimo cha korosho kuiona thamani yake.

Hata hivyo ameitaka serikali irejeshe utaratibu wa kuchangia pembejeo ili kwa mtu ambaye atashindwa kutoshelezwa na pembejeo inayotolewa bure awe tayari kuchangia kama mfumo wa zamani ulivyokuwa ukifanya. Mfumo huo ulikuwa ukitoa fursa ya wakulima kuchangia nusu ya mahitaji yao.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.