• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

BANDARI YA MTWARA KUPOKEA MELI KUBWA NA KUSAFIRISHA MAKAA YA MAWE KWENDA NJE YA NCHI.

Posted on: November 1st, 2021

MELI ya kwanza kubeba Makaa ya Mawe imewasili Bandari ya Mtwara kwa ajili ya kupakia tani elfu 33 za Makaa ya Mawe kwenda nchini India.

“APRILIA NASSAU”, Jina la meli hiyo yenye urefu wa mita 183 imewasili Oktoba 31 mwaka huu majira ya asubuhi na kupaki kwenye gati ya zamani huku ikitarajia kuondoka baada ya kukamilika kwa shughuli za upakiaji.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo la kupakia Makaa ya mawe hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Brigedia Jenerali Marco Gaguti amesema kuwa Meli hiyo ni ya kwanza kwa Bandari ya Mtwara kuanza kusafirisha Makaa ya Mawe na wanatarajia kusafirisha angalau tani elfu 40 kwa kila Meli.

Gaguti alisema Makampuni mengine ya usafirishaji yameonyesha nia ya kuja katika Bandari ya Mtwara kuingia kwenye biashara hiyo ya usafirishaji na kusafirisha Makaa ya Mawe hivyo upo uwezekano mkubwa wa kusafirisha zaidi ya tani elfu 40 kwa mwezi kutokea Bandari hiyo ya Mtwara.

“Kwa hiyo ni habari njema lakini pia tunafahamu umuhimu wa Bandari hii unakwenda kulinda miundombinu yetu ya nchi yetu lakini pia kupitia upande huu wa Kusini mwa Tanzania kutakuwa na ongezeko la mzunguko wa fedha, kutakuwa na ongezeko la ajira mbalimbali na hivyo kukuza uchumi wa Kusini lakini pia Mkoa wa Mtwara utaweza kukuza uchumi mkubwa katika nchini yetu”,Alisema Gaguti

Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Mtwara Mhandisi Juma Kijavara alisema kuwa, tayari wameshachukuwa tahadhari zote za kimazingira ikiwemo kuweka maturubai ili kupunguza chembe chembe za Makaa ya Mawe zinazoangukia Baharini au kuziondoa kabisa.

Pichani: Rc Marco Gaguti (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Mtwara Mhandisi Juma Kijavala

Hata hivyo amewatoa wasi wasi wasafirishaji ambao wanataka kutumia Bandari hiyo juu ya uwezo wa Bandari kwani zile tozo hazijapunguzwa kwa mzigo wa korosho tu bali ni kwa mzigo wowote utakaopitia Bandarini hapo kwahiyo ile asilimia 30 iliyopunguzwa kwenye tozo zao ni kwa ajili ya bidhaa yoyote inayopitia Bandarini hapo.

Katika hatua nyingine Meli ya mafuta imewasili katika Bandari hiyo yenye urefu wa mita 180 ambayo imepaki kwenye gati hiyo ya zamani ikiwa imeshusha mafuta zaidi ya lita Milioni 7 na gati hiyo kina chake ni kidogo kuliko gati mpya ambapo Bandari ina uwezo wa kufunga Meli kubwa zaidi ya Meli hizo mbali ambazo zimefunga Bandarini hapo kwa sasa.

“Kwahiyo uwezo upo na tunatarajia pia mizigo mingine kuendelea kuihudumia, tulikuwa tunaongelea kuwa tuna uwezo wa kufunga Meli nne kwa wakati mmoja leo mmeshuhudia Meli mbili zimefunga gati ya zamani na Meli mbili tuna uwezo wa kufunga gati jipya kwahiyo kama Bandari uwezo upo”,Alisema Kijavara

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Makaa ya Mawe ya Ruvuma Coal Limited Ryan Weinand alisema kuwa, Meli hiyo imakuja kwa majaribio kwani wanatarajia kuja kwa Meli nyingine Bandarini hapo wiki tatu zijazo.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.