Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

BANDARI YA MTWARA NI SALAMA;EPUKENI POROJO: Norbert Kalembwe, Kaimu meneja.

Posted on: December 12th, 2022

Kaimu Meneja wa Bandari ya Mtwara Norbert Kalembwe amewahakikishia wadau pamoja na wanainchi wanaoishi jirani na bandari hiyo kuwa shughuli zote zinazofanyika katika eneo hilo ikiwemo zile zinazohusisha kupokea na kusafirisha mizigo mbalimbali zinazingatia kanuni za afya na miongozo iliyowekwa kwa mujibu wa sheria kwa kuzingatia maslahi ya pande zote.


Kaimu Meneja Norbert Kalembwe ametoa kauli hiyo leo katika mkutano na waandishi wa habari bandarini hapo uliolenga kutoa ufafanuzi kuhusu  mikakati ya bandari katika kuhakikisha inazingatia miongozo na kanuni zilizowekwa wakati wa kuhifadhi na kusafirisha mizigo michafu (dirty cargo) bila kuathiri afya za wanainchi na mazingira.


Pia Kaimu Meneja ameongoza kuwa kutokana na hofu na sintofahamu iliyokuwepo bandarini hapo kuhusu suala zima la uhifadhi na usafirishaji wa makaa ya mawe, tayari uongozi umechukua hatua za haraka zenye maslahi kwa pande zote.

Kalembwe amesema kuwa kwa kuzingatia maslahi na afya za watumiaji wote wa bandari hiyo na jamii inayozunguka; bandari imeanza kufanya maboresho kwa kutenga eneo la kisiwa mgao kuwa gati mbadala litakalotumika katika usafirishaji wa makaa ya mawe pamoja na mizigo michafu (dirty cargo) hivyo kupunguza hofu ya usafirishaji wa mizigo yote katika gati moja.


Aidha Kaimu Meneja Norbert Kalembwe amesisitiza kuwa maboresho hayo yataleta mapinduzi makubwa katika bandari ya Mtwara kwa kulifanya eneo lililokuwa likitumika kusafirishia mizigo mchanganyiko kutumika kuhudumia mizigo mingine bila hofu.


Halikadhalika  Kalembwe ameongeza kuwa ili kuhakikisha bandari imepunguza athari za vumbi la makaa ya mawe kwa wananchi na wakazi wa maeneo jirani, uongozi wa bandari umeongeza vifaa maalum ikiwemo vinyunyizia mvuke (Spray canons), gari la kunyonya vumbi (Road sweeper truck), pamoja na nyavu za kupunguza kasi ya upepo kama njia ya kudhibiti athari zinazoweza kusababishwa na uhifadhi na usafirishaji wa mizigo ya aina hiyo.


Akihitimisha mkutano wake na wanahabari Kaimu Meneja Norbert Kalembwe ametoa wito kwa wadau wote wanaoitumia bandari ya Mtwara kuendelea kuitumia na kuiamini kwani ndio lango kuu la usafirishaji katika ukanda wa kusini huku akiwataka wakazi wanaoishi pembezoni na bandari kuondoa hofu kwani tayari serikali imeanza kutatua changamoto zote zilizokuwepo.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.