• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

BITEKO ATOA LESENI YA UENDELEZAJI WA KITALU CHA GESI, ATAKA WANANCHI WANUFAIKE KWANZA

Posted on: September 10th, 2024

Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Dotto Biteko leo tarehe 10/09/2024 ametoa Leseni ya Uendelezaji wa kitalu cha gesi cha Ruvuma, eneo la Ntorya, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara kwa kampuni ya Ara petroleum na Ndovu Resources kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Petroli (TPDC).

Akieleza faida zitakazopatika kutokana na leseni hiyo Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Ndg. Mussa Makame alisema mbali na kutumia gesi Kama nishati ya umeme pia wanatarajia kujenga kiwanda kidogo cha kuifanya gesi iwe kimiminika ambapo itatumika kwenye magari.

Mhe. Biteko amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyeruhusu leseni hiyo kutolewa kwani kwa mara ya mwisho leseni ya kuendeleza visima vya gesi ilitolewa mwaka 2006.

“Ni maagizo ya Mhe. Rais kuwa popote penye rasilimali na uwekezaji katika miradi mbalimbali basi wazawa wanufaike kwanza. Hivyo niagize kwenye mradi wa gesi TPDC ianze  kurudisha hisani kwa jamii (CSR) pia isisitize wakandarasi wake kufanya hivyo.” Alieleza Mhe. Biteko

Aidha, Mhe. Biteko ametoa maagizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ambako miradi  inatekelezwa kuhakikisha wanatenga kiasi cha pesa kutoka kwenye Ushuru wa Huduma (Service Levy) wanazopokea kutoka kwenye makampuni ili ziweze kutekeleza miradi ya maaendeleo badala ya kusubiri fedha kutoka Serikali  Kuu pekee.

Katika hatua nyingine Mhe. Biteko ameshuhudia utiaji saini Mkataba wa Maelewano (Memorandum of Understanding) baina ya TPDC na Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ambapo TPDC tayari imetenga kiasi cha shilingi Milioni 700 zitakazotumika kujenga kituo cha afya Dihimba ikiwa ni urudishaji wa hisani kwa jamii (CSR).


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.