• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Byakanwa kuwaongoza wadau kujenga shule Mtwara

Posted on: March 4th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Mhe. Gelasius Byakanwa amesema kipaumbele chake cha kwanza hadi cha tatu kwa mkoa ni elimu.

Aidha mkoa utajenga shule kwa kutumia michango ya kuchangia huduma za jamii (CSR) itakayosaidia kutatua changamoto za wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kufuata shule, pia kuondoa tatizo la  baadhi ya wanafunzi wanaorubuniwa na wazazi kufanya vibaya.

Byakanwa ameyasema hayo leo wakati akizungumza katika kikao cha wawekezaji na wafanyabiashara wa mkoani hapa na kusema ili mambo yote yaweze kwenda sawa elimu ni muhimu.

Amesema mkoa  wa Mtwara ulikuwa ukisuasua katika matokeo lakini kwa sasa umeanza kupiga hatua baada ya jitihada kubwa iliyohusisha wadau mbalimbali wa maendeleo.

“Nilipoingia hapa kwenye mkoa tulikuwa tunasuasua sana kwenye elimu, mwaka 2017 matokeo ya darasa la saba mkoa wa Mtwara ulishika nafasi ya 22 kati ya mikoa 26 lakini mwaka jana 2018 mkoa ni wanane katika mikoa 26 ya Tanzania, ni hatua kubwa,”amesema Byakanwa

Amesema katika matokeo ya darasa la nne pia mkoa ulishika nafasi ya nane kitaifa lakini changamoto iko katika matokeo ya kidato cha nne ambayo ilishika nafasi ya 25 kitaifa.

“Ukiangalia takwimu kiwango cha ufaulu kimeongezeka lakini nafasi ya mkoa kitaifa bado ni mbaya, kwanza tumeshuka..kwa mwaka 2017 tulikuwa nafasi ya 20 lakini mwaka jana tumekuwa nafasi ya 25,”amesema Byakanwa

Amesema zipo changamoto mbalimbali ikiwemo walimu na uhaba wa walimu lakini kama mkoa watakuja na mkakati kuendelea kukutana na walimu wa sekondari kuwekeana utaratibu kuona ni kwa namna gani wataongeza ufaulu kwa kidato cha nne kama ilivyo  elimu ya msingi.

Mshiriki wa kikao hicho, Hasnein Murji amesema wazo la kujenga shule ni zuri kwani itasaidia watoto wa mkoa huo kupata elimu.

“Sisi ndio watu wa Mtwara ni lazima tushirikiane kwa pamoja kuondoa changamoto zilizopo katika elimu ili kupiga hatua, tukitoa michango yetu na shule ikakamilika tutakuwa tumeweka alama,”amesema Murji

Mkazi wa Mtwara Ally Sudi amesema “Inapendeza kuona mkoa umekuja na wazo la kujenga shule kubwa kwa ajili ya wanafunzi itawasaidia kuondokana hata na vile vishawishi ambavyo vilikuwa vikiwasababishia kukatisha masomo sababu ya ujauzito lakini wavulana na wao hawatakuwa tena watoro,”amesema Sudi

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.