• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

CHANGAMKIENI FURSA SERIKALI IMEFUNGUA MILANGO KATIKA SEKTA YA KILIMO – MHE. KASSIM MAJALIWA MAJALIWA (MB) - WAZIRI MKUU.

Posted on: July 6th, 2023

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa( Mb) amesema serikali ya awamu ya sita tayari imeweka mikakati madhubuti ya kukuza sekta ya Kilimo nchini kama njia ya kumkwamua mkulima  na kumfanya aondokane na dhana ya Kilimo cha mazoea.


Mhe Waziri Mkuu Majaliwa ametoa kauli hiyo mjini Mtwara katika hafla ya Uzinduzi wa Ofisi za Benki ya Maendeleo ya Kilimo Kanda ya Kusini na kusema kuwa tayari serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 200 ambapo inatarajiwa kuona wakulima katika maeneo mbalimbali wananufaika na fursa hiyo.


Pia Mhe Waziri Mkuu Majaliwa ameongeza kuwa kufuatia ujio wa benki ya TADB Mkoani Mtwara anatarajia kuona Kasi ya Maendeleo inaongezeka na kuwavutia wawekezaji mbalimbali kuwekeza mkoani hapa.


Waziri Mkuu Majaliwa ameongeza kuwa serikali kwa kuthamini na kutambua umuhimu wa kuboresha sekta hii muhimu, tayari imeanza kuchukua hatua katika maeneo kadhaa yanayogusa sekta hiyo ili kuongeza tija.

''Ndugu wageni wote mlioshiriki katika hafla hii, napenda kuwahakikishia kuwa tayari serikali imeanza kuchukua hatua za kuboresha  mazingira ya wakulima, wafugaji pamoja na wavuvi" alisema Mhe Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.


Miongoni mwa maeneo ambayo Waziri Mkuu Majaliwa ameyataja kuwa serikali imeanza kuchukua hatua ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli na usafiri wa anga.

Ndugu wageni waalikwa, viongozi na watendaji wote naomba nichukue fursa hii kuwathibitishia kuwa serikali ya awamu ya sita kwa dhati kabisa imedhamiria kumkwamua mkulima katika Kanda ya Kusini" alisisitiza Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa.


"Miongoni mwa maeneo yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na kuongeza ruzuku ya pembejeo za Kilimo, ujenzi wa barabara ya kilometa  160 Kutoka Mnivata hadi Masasi, Maboresho ya Bandari ya Mtwara, ujenzi wa uwanja wa ndege Mtwara pamoja na ununuzi wa ndege kubwa ya mizigo jitihada ambazo ninaamini zikitumika kama ilivyokusudiwa zitaongeza tija katika eneo hili" aliongeza Waziri Mkuu Majaliwa.


Aidha Waziri Mkuu Majaliwa ameutolea Mfano mpango wa Mafunzo ya Kilimo kwa vijana unaojulikana kama Jenga Kesho iliyo Bora kuwa ni kielelezo cha jitihada za serikali  kumkwamua kijana kupitia sekta ya Kilimo na kusema kuwa mpaka sasa zaidi ya vijana 800 tayari wamepata mafunzo kupitia mpango huo.


Kwa upande wa sekta ya uvuvi ambayo ni miongoni mwa vyanzo vikuu vya mapato kwa Wananchi wa Mkoa wa Mtwara, Waziri Mkuu Majaliwa amesema serikali imetumia kiasi Cha shilingi bilioni 34 kuwajengea uwezo vijana ili waweze kuendesha shughili zao za uvuvi kwa tija katika ukanda wa Kusini katika Bahari ya Hindi.


Kufuatia Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Benki ya TADB Mkoani Mtwara, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa amewataka wadau mbalimbali kuitumia fursa hiyo kujikwamua kiuchumi halikadhalika kukuza pato la Taifa.


Awali alimkaribisha Mgeni rasmi katika hafla hiyo naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Hassan Chande ameutaka uongozi wa Benki hiyo kuepuka urasimu katika mchakato wa kutoa Mikopo huku Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Newala akihimiza umuhimu wa kutoa Elimu ya Mikopo kwa wakulima.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameishukuru serikali kwa kuupatia Mkoa wa Mtwara fedha nyingi za maendeleo ikiwemo zinazogusa sekta ya Kilimo na kuahidi kuwa serikali ya Mkoa itahakikisha zinatumika kama ilivyokusudiwa.


Ziara hiyo ya siku 6 ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) itaendelea tena kesho Julai 7, 2023 katika Halmashauri ya Manispaa- ya Mtwara Mikindani pamoja na Halmashauri ya Wilaya  ya Mtwara.


 MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.