• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Changamoto ya Salfa Mtwara kwisha,

Posted on: August 9th, 2017

Wananchi wakiwasilisha ujumbe wao kwa Serikali wakati wa maonesho ya Nanenane Ngongo


Changamoto ya upatikanaji wa salfa kwa ajili ya zao la mikorosho kwa mikoa ya Mtwara na Lindi litafikia mwisho Augosti 20 mwaka huu. Kuchelewa kwa salfa hiyo inayotolewa bure kwa wakulima wa maeneo haya lilitokana na kuchelewa kwa mipango ya ununuzi ambayo kwa sasa inakwenda vizuri.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. Charles Tizeba wakati akiwahutubia mamia ya wananchi wa mikoa ya Kusini waliohudhuria kwenye maonesho ya wakulima kitaifa maarufu kama Nanenane yaliyofanyika katika Viwanja vya Ngongo vilivyoko Manispaa ya Lindi Mkoani Lindi.

Mheshimwia Tizeba alikiri kuchelewa kwa usambazaji wa pembejeo hiyo ambapo amesema amesema tani ambazo zimeshaingia katika mikoa ya Lindi na Mtwara hadi sasa ni zaidi ya tani elfu 16 huku tani 2100 zilizobaki zikitarajiwa kuwasili julai 20 mwaka huu. Amesema mahitaji ya mikoa ya Mtwara na Lindi ni zaidi ya tani elfu kumi na nane.

Ametaja baadhi ya changamoto zilizochelewesha usambazaji wa pembejeo hizo kuwa ni pamoja na tatizo la takwimu za wakulima halisi wa mikorosho na idadi ya mikorosho waliyonayo. Anasema takwimu hizo ambazo hupatikana kutokana na vyama vya ushirika zilionesha mahitaji salfa kwa mikoa hii miwili ni zaidi ya tani 18,000 jambo ambalo walilifanyia kazi na kuagiza kiasi hicho.

Zaidi ya tani kumi na sita alfu zimeshafika nchini na kugawanywa kwa wakulima. Bado tani 2100 ambazo zimeingia bandarini jana na zinatarajiwa kusambazwa muda si mrefu na hivyo tatizo la pembejeo kwa mikoa ya Lindi na Mtwara litafikia mwisho.

Amezitaja baadhi ya changamoto kubwa zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa utoaji wa pembejeo bure kwa wakulima kuwa ni pamoja na wale waliokuwa wakinufaika na mfumo wa zamani ambao walikuwa wakiuza Salfa hiyo kwa bei ya juu kujiingiza kwa mbinu mbalimbali ili kuvuruga mfumo.

Pia wapo waliokuwa hawako katika mfumo ushirika wa vyama vya wakulima ambao baada ya utaratibu wa bure walijitokeza na kutaka kupata mgao. Hata hivyo Mheshimiwa Waziri ameagiza watu wenye sifa hiyo wasipewe kwani hawakuwa katika orodha ya idadi ya salfa iliyoagizwa.

Ameitaja changamoto nyingine kuwa wapo watu ambao wamekuwa wakichukua mifuko ya pembejeo iliyokwisha tumika wanaweka salfa ziliozpitwa na wakati na kuiuza madukani. Ameagiza viongozi wote wanaosimamia suala hilo kuwa makini ili kuhakikisha watu hao hawafanikiwi.

Awali akielezea mikakati ya serikali katika kuwakomboa wakulima, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema serikali imeweka mikakati imara ya kumkomboa mkulima. Ametaja mikakati hiyo kuwa  ni pamoja na kuondoa tozo zisizo za msingi ambazo walikuwa wakitozwa wakulima.

‘Kwa kutambua kuwa zaidi ya silimia 65.5 ya watanzania wanajihusisha na kujiajiri katika sekta ya kilimo, Ufugaji na Uvuvi  tumeendelea kuweka mipango kabambe ya kuhakikisha sekta hizi zinakua na wananchi wanafaidika nazo’. Alisema Makamu wa Rais.

Moja ya mikakati hiyo ni pamoja na kupunguza ushuru wa mazao, uliokuwa unatozwa na serikali za Mitaa kutoka asilimia 5 hadi asilimia 3 kwa mazao ya biashara na silimia 2 kwa mazao ya chakula.

Hatua nyingine ni kupiga marufuku utozaji wa ushuru kwa mazao yanayosafirishwa kutoka halsmahsauri moja kwenda nyingine ambayo uzito wake hauzidi tani moja. Amesema hizo zote ni njia za kumkomboa mkulimwa wa Tanzania.  

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.