• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

URUSI IKO TAYARI KUWEKEZA MTWARA – BALOZI ANDREY AVETISYAN

Posted on: September 8th, 2025

Balozi wa Urusi nchini Tanzania, Mhe. Andrey Avetisyan leo Septemba 8, 2025 amewasili mkoani Mtwara kwa ziara ya kikazi ya siku tatu ambapo anatarajiwa kutembelea miradi ya maendeleo katika wilaya za Mtwara Mjini na Vijijini pamoja na Newala.

Katika salamu zake za ukaribisho, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Sawala amemweleza Balozi Avetisyan kuwa serikali ya Mkoa inafungua milango kwa wawekezaji kutoka Urusi kuwekeza katika sekta viwanda vya kubangua korosho, uchumi wa bluu, nishati, kilimo na usafirishaji na kusisitiza kuwa serikali imeweka sera nzuri na rafiki zinazo walinda wawekezaji.

“Mhe. Balozi napenda kukuhakikishia kuwa serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inathamini na kuuenzi uhusiano wa nchi zetu mbili uliodumu kwa miongo kadhaa, hivyo kupitia Mkoa wetu wa Mtwara naomba uwafikishie salamu ndugu zetu wanaotaka kuwekeza Tanzania wanakaribishwa sana, fursa ziko nyingi tutawapa ushirikiano” alisema Kanali Sawala.


Kwa upande wake Balozi Avetisyan ameipongeza serikali ya Tanzania kwa sera bora za biashara na uchumi hatua ambayo amesema inaishawishi serikali ya Urusi kuwahamasisha raia wake kuutembelea Mkoa wa Mtwara na kuwekeza katika fursa zilizopo.

“Mhe. Mkuu wa Mkuu wa Mkoa binafsi ninafurahi sana kutembelea Mtwara, nimesikia ukielezea fursa nyingi na nzuri katika sekta mbalimbali, naomba kuchukua fursa hii kukuhakikishia tuko tayari kushirikiana na nyinyi, katika sekta za ujenzi wa barabara, viwanda vya kuchakata mbolea na gesi,usafirishaji majini pamoja na kandarasi za ujenzi wa barabara, maeneo yote haya tuna wataalamu na teknolojia ya kisasa” alisisitiza balozi Andrey Avetisyan.

Kuhusu ushirikiano katika sekta ya elimu Balozi Andrey Avetisyan amesema serikali ya nchi hiyo hivi sasa imeongeza nafasi za wanafunzi wanaokwenda kusoma fani mbalimbali huku akiwataka wanafunzi wenye sifa kutoka Mtwara kuitumia fursa hiyo.

Katika siku ya kwanza ya ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Urusi Mhe. Andrey Avetisyan mkoani Mtwara ametembelea bandari ya Mtwara, Kongani la viwanda vya korosho katika Halmashauri ya Mji Nanyamba pamoja ofisi za Bodi ya korosho mjini Mtwara.

Aidha Balozi Avetisyan amesema kuwa Ujumbe wake umevutiwa na mradi wa ujenzi wa Kongani la Viwanda vya kubangua korosho katika Kijiji cha Maranje katika Halmashauri ya Mji Nanyamba ambapo amesema wanakusudia kuitangaza fursa hiyo nchini Urusi ili iweze kuzinufaisha pande zote mbili.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MSIMU WA 4 WA MADAKTARI WA SAMIA; MTWARA YAPEWA MADAKTARI BINGWA 54

    September 15, 2025
  • CAG ZIARANI MTWARA; AIPONGEZA OFISI YA MKUU WA MKOA KWA KUPATA HATI SAFI

    September 15, 2025
  • BALOZI WA URUSI AVUTIWA NA UTALII MTWARA

    September 10, 2025
  • “KALAMU YA MWANA HABARI INA NGUVU, ITUMIKE VIZURI” RC SAWALA

    September 10, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.