Benki ya CRDB Kanda ya Kusini imetoa msaada wa Sare za Michezo ‘Tracksuits’ Jozi 120 kwa timu ya UMISSETA ya Mkoa wa Mtwara kwaajili ya Maandalizi ya Mashindano ya UMISSETA Taifa yanayotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao.
Akipokea Jozi hizo kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Afisa Elimu Mkoa, John Lupenza, aliishukuru Benki hiyo na kuahidi kuwa Timu hiyo itafanya vizuri katika Mashindano hayo.
CRDB iliwakilishwa na Meneja Biashara CRDB Bank Kanda ya Kusini, Emmanuel Biganio akiwa na Mbwana Ahmed ambaye ni Meneja wa Tawi la CRDB Mtwara, Sambamba na Meneja Mahusiano Kitengo cha Serikali - CRDB Kanda ya Kusini, Alpha Mhagama.
Kwa mujibu wa Afisa Michezo Halmashauri ya Manispaa-Mikindani, Mack Kayombo ilisema Michezo ya UMMISETA mwaka huu inatyarajiwa kufanyika Mkoani Iringa kuanzia tarehe 07 Juni, hadi 30 Juni 2025.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara
Anuani ya Posta: 544, MTWARA
Simu: +255 23 2333014
Mobile: +255 23 2333014
Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz
Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.