• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

EPUKENI MIGOGORO YA KIFAMILIA MNA WAADHIBU WATOTO WASIO NA HATIA – DKT GWAJIMA

Posted on: April 11th, 2025

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalumu Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wazazi na walezi kuepuka migogoro na mifarakano katika familia ili kupunguza wimbi la Watoto wanaoishi mtaani.

Dkt. Gwajima ametoa kauli hiyo katika mdahalo wa maandalizi ya kilele cha Siku ya Kimataifa ya Mtoto anayeishi na kufanya kazi Mtaani uliofanyika katika Ukumbi wa VETA mjini Mtwara ambapo amesema katika siku za hivi karibuni baadhi ya wazazi wamejenga utamaduni wa kuzua migogoro inayosababisha ongezeko la talaka ambazo zimechangia ongezeko la watoto wa mitaani.

“Bila shaka nyote ni mashahidi wa matukio yanayoendelea katika jamii yetu, yaani huko ni purukushani tupu, leo mzazi huyo kamfukuza mkewe kesho mwingine anaomba talaka yaani kwa ujumla hali si shwari” alisema Waziri Gwajima.

Kufuatia hali hiyo Waziri Gwajima ameitaka jamii kuhakikisha inarejea katika misingi ya malezi kwa Watoto ambao ni kizazi cha kesho ili kuepuka vitendo vya mmomonyoko wa maadili ambavyo vinachangia ongezeko la Watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani.

“Ndugu washiriki wa kongamano hili nimemsikia Mkuu wenu wa mkoa akisema kuna idadi ndogo ya watoto wanaoishi mtaani ambao hawazidi tisini, kwa ujumla hii ni habari njema, lakini naomba msibweteke endeleeni kuweka mikakati ya kuzuia ongezeko, kataeni mila na desturi kandamizi pia watumieni maafisa usawi wa jamii kutatua migogoro, halikadhalika jielimisheni kupitia maafisa maendeleo ya jamii kuhusu fursa za kiuchumi ikiwemo mikopo ya riba nafuu, kwa ujumla hatua hii itapunguza migogoro katika jamii” alisisitiza Dkt. Gwajima.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Sawala amesema mkoa unaendelea kuweka mikakati endelevu ya kuondokana na tatizo hilo ikiwemo kutoa elimu kwa wazazi na walezi kupitia maafisa ustawi wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwapa Watoto malezi bora sambamba na kuhakikisha unalinda haki za Watoto kama sheria inavyoelekeza.

Maadhimisho hayo yaliyobebwa na kauli mbiu “Imarisha ushirikiano kuzuia Watoto kuishi mtaani” yanafikia kilele chake hapo kesho mjini Mtwara.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU 2025 KUPOKELEWA MKOANI MTWARA MEI 17

    May 15, 2025
  • MTWARA TUKO TAYARI KUUPOKEA NA KUUKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025

    May 14, 2025
  • UFUTA NA MBAAZI KUPIMWA KIDIGITALI MKULIMA KUPATA RISTI KUPITIA SIMU YAKE

    May 14, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE. KANALI PATRICK SAWA AKAGUA MRADI WA MAENDELEO TANDAHIMBA

    May 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.