• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

IGENI MFANO WA MTWARA KUBORESHA ELIMU – WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA, PROF ADOLF MKENDA.

Posted on: March 16th, 2023

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameziagiza taasisi zinazoshughulika na maswala ya Elimu pamoja na wadau kuiga mfumo wa kuboresha sekta ya Elimu unaotumiwa na MKoa wa Mtwara na kusema kuwa unaonyesha dira ya kuikomboa sekta ya Elimu.

Katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Naibu Waziri wake Omari Kipanga aliyemwakilisha, imesema kuwa Serikali inatambua jitihada mbalimbali zinazofanywa na mkoa wa Mtwara katika kuboresha mfumo wa ufundishaji na ujifunzaji hivyo itaendelea kuunga mkono jitihada hizo kwa kuboresha miundombinu na pia kuwawezesha watendaji.

Akikabidhi zawadi na vyeti kwa washindi katika Kilele Cha juma la Elimu mjini Mtwara, wakiwemo walimu, wanafunzi na wadau wa Elimu waliofanya vizuri katika mwaka wa masomo wa 2022/2023 Naibu Waziri Kipanga amesema utaratibu huo wa motisha utaongeza ari ya kufanya vizuri zaidi kwa walimu na wanafunzi mashuleni na hivyo kuufanya Mkoa kushika nafasi ya juu katika matokeo ya mitihani.

" Binafsi naomba nichukue fursa hii kuwapongeza sana kwa kubuni mfumo huu mzuri wa motisha katika Elimu, ninawaahidi nitakuwa Balozi wenu mzuri huko niendako kwa kuwahamasisha wadau mbalimbali kuwatembelea na kuiga mikakati mnayoitumia " alisema Naibu Waziri Kipanga.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed alimweleza mgeni rasmi kuwa baada ya kuanza kutumia utaratibu huo wa Motisha matokeo ya mitihani katika ngazi zote yameboreka tofauti na miaka iliyopita.

" Ndugu mgeni rasmi, kwanza kabisa ninaomba nichukue fursa hii kuipongeza serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuupatia Mkoa wetu fedha nyingi zinazogharimia sekta ya Elimu, sisi wanamtwara tunamuahidi tutasimamia kikamilifu sekta hii ya Elimu Ili tuweze kuandaa vijana watakaokuwa tegemeo la kesho" alisisitiza Kanali Ahmed Abbas Ahmed.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Abdallah Malela amewashukuru wadau waliofanikisha kupatikana kwa tuzo hizo zilizogharimu kiasi cha shilingi Milioni 143 yakiwemo magari 2 aina ya Noah, Pikipiki 13 ,baiskeli pamoja na fedha taslimu.

"Ndugu mgeni rasmi, naomba nizishukuru kwa dhati kabisa taasisi zote zilizochangia kufanikisha shughuli hii, bila kuwasahau wadau wetu wakuu TANECU na MAMCU, halikadhalika Benki ya CRDB pamoja na Dangote, tunawashukuru sana" alisema Katibu Tawala Abdallah Malela.

Katika tuzo hizo halmashairi ya Wilaya ya Newala imeibuka mshindi wa jumla ambapo imepata magari mawili aina ya Noah yenye thamani ya shilingi Milioni 50 huku walimu 8 wakizawadiwa Pikipiki na wengine fedha taslimu.

                                                                                                                                               

MWISHO.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2022 November 24, 2021
  • Majina ya watumishi wa umma wanaostahili kulipwa madai ya malimbikizo February 09, 2018
  • KUFANYA MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19 August 30, 2021
  • Matokeo ya Kidato cha NNe 2017 January 30, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • IGENI MFANO WA MTWARA KUBORESHA ELIMU – WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA, PROF ADOLF MKENDA.

    March 16, 2023
  • TUONGEZE JITIHADA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA: KANALI AHMED ABBAS AHMED

    March 08, 2023
  • NIMERIDHISHWA NA UBUNIFU WA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU¬_WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU MHE. PROF JOYCE NDALICHAKO.

    March 06, 2023
  • LETENI MAONI YENU TUTABORESHA MFUMO WA UTOAJI HAKI_JAJI MKUU MSTAAFU OTHMAN CHANDE.

    February 28, 2023
  • Tazama Zote

Video

Wakulima Mtwara wachangamkia kilimo cha Ufuta
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • NBS
  • IKULU
  • UTUMISHI
  • SALARY SLIP
  • e-GA

Kurasa Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.