• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA YAZINDULIWA MKOA WA MTWARA; HUDUMA KUTOLEWA BURE

Posted on: January 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Sawala leo tarehe 24 Januari 2025 amezindua kampeni ya msaada wa kisheria ya mama Samia (Samia Legal Aid Campaign) yenye lengo la kuhakikisha mifumo ya haki inaimarishwa na kwamba makundi yasiyokuwa na uwezo hususan wanawake na watoto wanaifikia haki kupitia huduma za msaada wa kisheria.

“Kampeni hii imekuwa ni mkombozi kwa wanyonge hususani wale wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za mawakili na kwamba inapunguza kwa kiasi kikubwa malalamiko ya wananchi katika sekta ya sheria na kupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani na katika vyombo vingine vya haki.” Alieleza Kanali Sawala

RC Sawala aliendelea kueleza kuwa kampeni hiyo inatekeleza falsafa ya 4R ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambazo ni Maridhiano (Rencoliation), Ustahimilivu (Resiliance), Mageuzi (Reforms), na Kujenga Upya Taifa (Rebuilding) ambazo ni misingi imara ya utawala wa sheria na utaoaji haki.

Kwa upande wake Mwakilishi wa naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Abraham Mshamu alieleza kuwa kutakuwa na utolewaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa siku 9 katika Halmashauri zote tisa za Mkoa na katika ngazi ya Kata, Vijiji na Mitaa ambapo huduma zote zitatolewa bure.

Mwaka 2017 Serikali ilipitisha Sheria ya Msaada wa Sheria, Sura ya 21. Sheria hii imeazimia kuwasaidia wanyonge ambao hawana uwezo wa kifedha na hawana uelewa wa masuala ya sheria.

Huduma zitakazotolewa ni pamoja na elimu na ushauri katika masuala ya migogoro ya umiliki wa ardhi, mirathi, Ukatili wa Kijinsia hususan kwa wanawake na watoto, Matunzo ya watoto; na masuala ya ndoa.

Aidha, Wakala wa Usajili Ufilisi Udhamini (RITA) katika kampeni hiyo ya msaada wa kisheria ya mama Samia watatoa huduma za vyeti vya kuzaliwa, vifo na uandishi wa wosia huduma.

Kauli Mbiu ya Kampeni hii ni “Msaada wa Kisheria kwa Haki , Usawa, Amani na Maendeleo”.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.