• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Katibu Mkuu awataka Wadau wa Elimu kushirikiana kutatua changamoto za elimu

Posted on: April 29th, 2017

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Dkt.Leonard Akwilapo akikagua moja ya mabanda ya maonesho wakati wa kilele cha maazimisho ya wiki ya Elimu Kitaifa tukio lililoadhimishwa Mkoani Mtwara jana


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Dkt.Leonard Akwilapo amewataka wadau wote wa elimu kuwa sehemu ya utatuzi wa changamoto za elimu hapa nchini. Hayo amesema jana wakati akifunga Juma la Elimu Kitaifa lililofanyika shule ya Sekondari Mangaka iliyoko Wilayani Nanyumbu mkoani Mtwara.

Dkt. Akwilapo amesema changamoto za elimu ni nyingi hivyo zinapaswa kutatuliwa kwa ushirikiano wa kila mdau. Ameyataja baadhi ya masuala muhimu yanayopaswa kupewa kipaumbele kwa kipindi hiki kuwa ni pamoja na uimarishaji na usimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji ambapo Walimu, Wadhibiti Ubora wa Elimu, Viongozi wa Halmashauri na wadau wote wa Elimu wanapaswa kuhakikisha wanatumia nafasi zao kuondoa changamoto hizo.

Katika sherehe hizo zilizoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) Akwilapo amesema kwa sasa ufaulu wa shule zisizo za serikali hapa nchini zinaongoza. Siri kubwa ya ufaulu huo ni usimamizi mzuri jambo ambalo hata serikali inaweza iwapo kila mdau ataamua kuwajibika katika sehemu yake.

‘Kama serikali tunapaswa kuangalia na kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi. Walimu wanaofundisha serikalini na shule za binafsi ni walewale na wamesoma vyuo vilevile, lakini wanapoenda shule binafsi wanafanya vizuri. Kwa nini wasifanye vizuri hata wanapokuwa katika shule za serikali’? Amesema Akwilapo.

Aidha, Dkt. Akwilapo amekemea tabia ya baadhi ya walimu kufanya kazi binafsi nyakati za masomo wakiwemo wale wanaoendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda. Amesema hiyo ni moja ya sababu zinazokwamisha maendeleo ya elimu hapa nchini. Amewataka Wadhibiti ubora wa shule waboreshe njia za kufanya tathimini. Badala ya kuanza kutoa taarifa kwa walimu kabla ya kwenda kuwakagua, wawe na utaratibu wa kuvamia ili kuwabaini walimu wanaotoka kwenye vituo vyao vya kazi kabla ya wakati. Hilo litasaidia kuwafanya walimu wawe tayari muda wote.

Pia wadhibiti ubora wawe na kumbukumbu ya watu waliokwisha wakagua badala ya kujikuta wanamkagua mwalimu mmoja tu kila wanapotembelea shule husika.

Kwa upande wake Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Kathleen Sekwao amemtaka Katibu Mkuu kuhakikisha mkoa wa Mtwara na hasa wilaya ya Nanyumbu inaangaliwa kwa jicho la pekee ili kutatua changamoto nyingi zilizopo. Amesema wao kwa upande wao watahakikisha wanautangaza mkoa kwa wadau mbalimbali ili wasaidiane na wenyeji katika kuinua kiwango cha elimu.

Pia ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kutatua changamoto mbalimbali za elimu kama vile kuongeza bajeti kulinganna na mahitaji yakiwemo mahitaji ya watoto wenye mahitaji maalumu. Na kutoa motisha kwa walimu wanaofanya kazi katika mazingira magumu

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.