• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Kila mtanzania kupata BIMA ya Afya

Posted on: February 27th, 2019

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustin Ndugulile akimkabidhi Said Akili, mwanachama wa chama cha Msingi Nyundo B, kijiji cha Nyundo, Halmashauri ya Wilya ya Nanyamba kadi ya uanachama wa Bima  ya Afya (Ushirika Afya) mara alipotembelea katika Ofisi za Bima ya Afya (NHIF) mjini Mtwara jana Februali 26, 2019.


Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea na taratibu za kuhakikisha kila mtanzania anafikiwa na huduma ya Bima ya Afya. Akizungumza jana wakati wa ziara ya kikazi mjini mjini Mtwara Naibu Waziri wa Afya Mhe. Faustin Ndugulile amesema lengo lao ni kuhakikisha mwaka huu 2019 zoezi hilo muhimu kwa afya ya watanzania linatekeklezwa.

 “Kubwa ambalo serikali tumepanga kulifanya mwaka huu ni kuhakikisha kila mtanzania anapata Bima ya Afya. Hili  ni agizo la Mheshimiwa Rais kuhakikisha kila mtanzania hahangaiki na huduma ya afya na badala yake atembee na kitambulisho kinachomuwezesha kupata huduma hiyo.”  Amesema Mhe. Ndugulile

Amesema hadi sasa serikali imeendelea na maboresho katika huduma mbamimbali za Bima ikiwemo CHF iliyoboreshwa inayomuwezesha mwanachama kupata huduma ya afya kwenye vituo mbalimbali tofauti na ile ya awali ambayo ilikuwa ikimuwezesha mwanachama kupata huduma kwenye kituo kimoja tu.

Pia huduma ya Ushirika Afya ambayo inalenga kuwafikia wakulima walioko katika vyama vya ushirika vya mazao mbalimbali. Mheshimiwa Naibu Waziri amempongeza ndugu Said Akili, mkulima wa korosho kutoka kijiji cha Nyundo katika chama cha Msingi Nyundo B kwa kutambua umuhimu wa Ushirika Bima na kujiunga. Aidha amesema Ushirika Bima inapatikana kwa shilingi 76,800 kwa mwaka na inamuwezesha mwanachama kupata huduma ya afya kwenye vituo zaidi ya elfu sita nchi nzima.

 Amesema hizi huduma zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto za huduma za afya. Kinachotakiwa sasa ni kuhamasiha wananchi kujiunga na bima hizi kwani zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuondokana na changamoto hizi.

Kwa upande wake Said Akili amewataka wakulima wenzake kuchangamukia huduma hiyo kwani changamoto za wakulima ni ninyingi.

“Wakulima wengi tunatumia jembe la mkono na Panga na tunakuwa na fedha kipindi cha miezi ya mauzo. Baada ya hapo wengi tunakuwa hatuna fedha. Bahati mbaya ugonjwa hauchaguai muda hivyo ukiwa na kadi ya Bima itasaidia kupata huduma ya afya bila wasiwasi”. Amesema Said

Mhe. Ndugulile amekuwa na zira ya siku mbili mkoani hapa ambapo ametembelea maeneo mbalimblai ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Ligula, Hospitali ya Kanda ya Kusini inayojengwa mjini Mtwara, Ofisi za Bandari Mtwara pamoja na ofisi za Bima ya Afya Mtwara.

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.