• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

KUWENI WAZALENDO WEKENI MASLAHI YA TAIFA MBELE _ Dunstan Kyobya, Mkuu wa wilaya ya Mtwara.

Posted on: December 16th, 2022

Mkuu wa wilaya Mhe. Dunstan Kyobya amewaasa wahitimu wa kozi ya mafunzo ya jeshi la akiba kuutunza ujuzi waliopata kudumisha amani na kutetea maslahi ya Taifa.

Mhe. Kyobya ametoa wito huo katika hafla ya kufunga mafunzo ya jeshi la akiba iliyofanyika katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara na kusema kuwa serikali ina matumaini makubwa kuwa wahitumi hao watakuwa mfano wa kuigwa katika jamii.

"Ndugu wahitimu wa kozi hii ya jeshi la akiba, leo ni siku yenu muhimu inayoingia katika kitabu cha historia ya maisha yenu" alisema Kyobya.


"Nimeambiwa awali wakati mnaanza kozi hii mlikuwa 212, lakini kwa bahati nzuri 14 wakachaguliwa kujiunga na jeshi la kujenga Taifa, bila shaka hii ni faraja kubwa kwetu, sasa na nyinyi hakikisheni mnazingatia miiko na maadili mliyofundishwa na wakufunzi wenu itawasaidia kuaminika" alisema Mhe. Kyobya.

Halikadhalika Kyobya amesisitiza kuwa serikali inatarajia kuwa wahitimu hao watakuwa mabalozi wazuri wa mafunzo hayo na kujijengea imani na heshima katika jamii huku akiwataka kuweka mbele suala la uzalendo, uadilifu na nidhamu.


Pia Mhe. Dunstan Kyobya amelitumia jukwaa la hafla hiyo kuwahakikishia wahitimu kuwa, serikali inatambua changamoto ya ajira inayowakabili na kusema kuwa tayari Uongozi wa Wilaya na Mkoa unafanya jitihada za kuwasiliana na vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na taasisi zenye mahitaji ya vijana wenye sifa za mafunzo ya aina hiyo ili watoe kipaumbele katika ajira pindi zitakapojitokeza.

Jumla ya wahitimu 198 wametunukiwa vyeti vya kozi ya mafunzo ya  miezi 6 ya Jeshi la akiba yaliyoanza mwezi Julai  Mwaka huu ambapo kati ya hao 144 ni wanaume na 54 ni wanawake.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.