• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mashamba Darasa Ufuta kuanzishwa Mtwara

Posted on: June 12th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele kuanzisha mashamba darasa ya ufuta mkoani hapa.

Agizo hilo amelitoa leo Juni 12, 2019 wakati akizindua mafunzo ya matumizi sahihi ya viuatilifu  kwa wakulima na Maafisa Ugani katika kijiji cha Maili Kumi wilayani Mtwara. Amesema mashamba hayo yatasaidia kutoa elimu kwa wakulima wa ufuta na hivyo kuongeza uzalishaji wa zao hilo. Pia, itapanua uelewa wa teknolojia ya kilimo na kuachana na imani ya baadhi ya wakulima kuwa shamba la ufuta linahitaji kupumzishwa kila baada ya msimu mmoja wa kilimo.

Amezitaja baadhi ya wilaya ambazo zinaweza kuanzishwa mashamba hayo ambayo yatamilikiwa na Halmashauri kuwa ni Masasi, Nanyumbu na Mtwara.

“Dkt. Kapinga, Tunahitaji kuwa na shamba la mfano. Wasiliana na halmashauri ya Masasi tupate shamba kubwa la halmashauri ambalo tutalisimiamia kuonesha kilimo cha ufuta, Pia Nanyumbu na Mtwara.” Amesema Byakanwa.

Amesema ardhi ya kilimo cha ufuta ipo ya kutosha hivyo ni suala la wakulima kuwezeshwa elimu. Amesema kwa sasa mkoa umedhamiria kuendeleza kilimo hicho ambacho kimeingizwa katika mfumo wa stakabadhi ghalani kama ilivyo kwa zao la korosho.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendelea (TARI–Naliendele) Dkt. Fortunatus Kapinga amesema Taasisi iko tayari kutekeleza agizo hilo. Amesema kilimo cha mazao mbadala imekuwa ni moja ya maekezo yao kwa wakulima wanakapoanzisha mashamba mapya ya korosho hivyo ni suala la kuweka msisitizo na kuongeza elimu zaidi.

Mkoa wa Mtwara ni moja ya wazalishaji wakuu wa zao la korosho ambalo limekuwa likiuzwa kupitia utaratibu wa stakabadhi ghalani. Msimu wa 2019/2020 zao la ufuta pia limeingizwa katika utaratibu huo jambo ambalo linawafanya viongozi wa mkoa kuhakikisha wanasisitiza wakulima kuchangamkia zao hilo.


video yake hii HAPA

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.