• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MWENGE WA UHURU MASASI

Posted on: May 18th, 2025

Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Mtwara leo Mei 18, 2025 zimeingia katika siku yake ya pili ambapo Mwenge umetembelea, umekagua, umeweka mawe ya msingi na kuzindua miradi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 3.5 katika Halmashauri ya Mji Masasi.

Mapema asubuhi Mwenge wa Uhuru uliweka jiwe la msingi katika Mradi wa Ujenzi wa barabara ya Nyasa shuleni yenye urefu wa kilometa 1 yenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 456 na baadae kuona na kukagua shughuli za vijana wa kikundi cha Jitihada Nyasa Chini.

Halikadhalika Mwenge wa Uhuru umezindua Mradi wa Ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo katika Shule ya msingi Mkuti wenye thamani ya Shilingi milioni 83.4 na baadae Mwenge ulizindua nyumba ya watumishi wa afya katika kituo cha Afya Mtandi wenye thamani ya Shilingi milioni 95.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi na uwekaji wa mawe ya msingi katika miradi hiyo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Ismail Ali Ussi amesema ameridhishwa namna miradi hiyo ilivyotekelezwa Kwa kiwango.

" Ndugu wanamasasi nichukue fursa hii kuwapongeza Kwa hatua hii nzuri ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo, nimejionea miradi yenu ya barabara, Ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja nyumba za watumishi wa afya kwa ujumla miradi imekidhi ubora wa viwango hongereni Sana" aliongeza Ndugu Ismail Ali Ussi.

Aidha Ndugu Ismail Ali Ussi pia ameiagiza Halmashauri ya Mji wa Masasi kuangalia uwezekano wa kupanua wigo wa kutoa mikopo Kwa utaratibu wa asilimia kumi yenye riba nafuu kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi.

Kuhusu umuhimu wa wananchi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura Kiongozi wa Mbio za Mwenge Ismail Ali Ussi amewataka viongozi kuwahamasisha wananchi wenye sifa kuhakiki taarifa zao na wale ambao hawajajiandikisha kujiandikisha Ili waweze kupata haki ya kuwachagua viongozi wao katika uchaguzi mkuu ujao.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.