• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2024 MKOANI MTWARA ZAKAMILIKA

Posted on: June 8th, 2024


Leo Juni 8,2024 Serikali ya Mkoa wa Mtwara imekabidhi Mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Sauti moja Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma kwa ajili ya kuendelea na mbio zake mkoani humo.

Akizungumza mkoani Ruvuma kwenye  kukabidhi Mwenge huo, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Kenan Sawala amesema Mwenge umepitia miradi 62 mbalimbali ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 30 ukiwa mkoani Mtwara.

Pia umekimbizwa katika njia zenye urefu wa kilomita 906.6 kwenye Halmashauri zote 9 na kuweka mawe ya msingi miradi 22, kufungua miradi 2 na kuzindua miradi 11.

Aidha, Mwenge umeona na kukagua miradi 27 inayotekelezwa na  wananchi kwa kushirikiana na Serikali Kuu, wahisani, pamoja na Halmashauri kuwa ujumla.

"Miradi hii yote iliyokamilika na mingine mingi ambayo inaendelea katika mkoa wetu ni kazi kubwa ya Mhe. Dkt. Rais Samia Suluhu Hassan, sisi kama Mtwara tunashukuru sana kwa kutupatia fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya mkoa wetu."amesema Kanali Sawala.

Kwa upande wake Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Eliakimu Mnzava ameridhika na utekelezaji wa miradi katika mkoa huu wa Mtwara na kupongeza namna ambayo fedha nyingi  zinazotolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji huo  zilivyotendewa haki.   

Aidha, amewataka viongozi kuendelea kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo bado haijakamilika na tayari imewekwa jiwe la msingi ili iweze kukamilishwa vizuri.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema Mwenge ukiwa mkoani humo utakimbizwa katika Halmashauri 8 na kutembelea miradi 72 mbalimbali ya maendeleo nyenye thamani ya zaidi ya Sh. Bilioni 46.

Pia utakimbizwa umbali wa kilomita 1289.50 na utafungua miradi 17, miradi 13 kuwekewa mawe ya msingi na miradi 42 itatembelewa, kukaguliwa.

Aidha Mwenge huo kwa mkoa wa Mtwara ulipokelewa Mei 30,2024 katika kijiji cha Mpapura Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara na Juni 7, mwaka huu umemaliza mbio zake ndani ya mkoa huo.



ASANTE NA KILA LA KHERI MWENGE WA UHURU 2024.



Juni 8, 2024.



#TunaifunguaMtwara

#KaziIendelee


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.