• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MBIO ZA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MJI NANYAMBA MKOANI MTWARA

Posted on: June 1st, 2024


Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Mtwara Leo  tarehe 1 Juni 2024 umeanza ziara yake katika Halmashauri ya Mji Nanyamba Wilayani Mtwara.

Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Halmashauri hiyo umeweka jiwe la msingi, umezindua pamoja na kutembelea na kuona jumla ya Miradi 7 yenye thamani ya shilingi Bilioni 7.73

Mradi wa kwanza ulikuwa mradi wa vyumba viwili vya madarasa wenye thamani ya shilingi Milioni 48.3  katika shule ya msingi Maranje.

Akizungumza mara baada ya ufunguzi wa mradi huo Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndg. Godfrey Mzava ameipongeza Halmashauri ya Mji Nanyamba kwa kusimamia vizuri matumizi ya mfumo mpya wa Manunuzi wa NEST na kusema kuwa unasaidia kuondoa mianya ya ubadhilifu na upendeleo katika utoaji zabuni.

Mara baada ya zoezi Hilo Mwenge wa Uhuru ulielekea Kijiji Cha Chawi kukagua shamba la Miti la mjasiliamali . Saada ni Nankaha ambapo Mhe. Godfrey Mzava amewataka viongozi na wadau wa Mazingira kuhakikisha  wanahamasisha  wananchi kupanda miti Ili kutunza Mazingira kama kauli mbiu ya Mwenge ya mwaka huu inavyosisitiza.

"TUNZA MAZINGIRA NA SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA UJENZI WA TAIFA ENDELEVU"

Mradi mwingine uliotembelewa na Mwenge ni mradi umeme  wa REA ambapo kiongozi wa Mwenge alikagua na kuona zoezi la uwashaji wa umeme  eneo la Chawi sokoni katika nyumba ya mzee Mohamed Hamis ambapo alishiriki kuwasha umeme katika nyumba hiyo, zoezi linaloashiria umuhimu wa Serikali kuwekeza shilingi Bilioni 22 kusambaza umeme katika vijiji vya Halmashauri ya Mji Nanyamba huku akiwataka wananchi kuitunza Miundombinu ya Mradi huo.

Akiwa  katika  shule ya  msingi Chawi  Kiongozi wa Mbio za Mwenge Mh. Mzava alikagua na kuona shughuli za Banda la Mazingira, alikagua  Banda la Afya na Lishe  pamoja na kuzindua klabu ya wapinga rushwa.

Kisha Mwenge wa Uhuru ulikagua hatua ya Mradi wa uendelezaji wa Zahanati Mkomo katika Kijiji Cha Mkomo Uliogharimu kiasi Cha shilingi Milioni 9.9.

Akiwa katika  Zahanati hiyo  kiongozi wa Mbio za Mwenge Mhe. Godfrey Mzava ameiagiza Halmashauri  hiyo kukamilisha Ujenzi wa Miundombinu  ikiwemo kuweka mfumo wa kuvuna maji ya  mvua  pamoja na kujenga kichomea taka Ili kurahisisha mchakato wa utoaji huduma.

Katika mtaa wa Kilimanjaro katika Mji wa Nanyamba Mwenge wa Uhuru uliweka jiwe la katika Mradi wa Ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa kilometa moja  uliopewa jina  Hawa Ghasia Road  Uliogharimu  kiasi Cha shilingi  Milioni 450.

Katika Mradi huo Mhe. Mzava ameutaja  kuwa ni kielelezo jitihada za Serikali katika kuboresha Miundombinu ya usafirishaji na kuwataka wananchi kuitunza barabara hiyo.

Aidha Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndg. Godfrey Mzava ameipongeza Wakala wa Barabara Vijijini TARURA kwa kukidhi vigezo vya mfumo Mpya wa Manunuzi  NEST kama ambavyo sheria inawataka na kusema kuwa hicho ni miongoni mwa vigezo ambavyo vimechangia kufanikisha utekelezaji wa Mradi huo.


Juni 01, 2024

#TunaifunguMtwara

#KaziIendelee


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA.

    June 24, 2025
  • MKURUGENZI MPYA NANYAMBA NA DAS MPYA MTWARA WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

    June 23, 2025
  • MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA UTEGEMEZI KWA WAFADHILI.

    June 28, 2025
  • MAREKANI KUTUMIA BANDARI YA MTWARA KUSAFIRISHA BIDHAA

    June 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.