• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MBIO ZA MWENGE WA UHURU MKOANI MTWARA ZABISHA HODI WILAYANI NEWALA

Posted on: June 3rd, 2024

Mwenge wa Uhuru leo Juni 03, 2024 umeanza mbio zake Wilayani Newala ambako umezindua Miradi, umeweka mawe ya msingi pamoja na kutembelea, kukagua na kuona miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Mji wa Newala.

Ukiwa Katika Halmashauri hiyo Mwenge wa Uhuru umetembelea miradi 7 yenye thamani ya. Shilingi bilioni 4.25.

Mradi wa kwanza kutembelewa ulikuwa  ni mradi wa ujenzi wa barabara ya makondeko hadi Mkunya kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 2 katika kijiji Cha Makondeko iliyogharimu kiasi Cha shilingi Milioni 949.9.

Akiweka jiwe la msingi katika mradi huo kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Godfrey Mzava amemwagiza Wakala wa Barabara Vijijini TARURA kuhakikisha wanaweka mipaka  inayotambulika kisheria kati ya barabara na makazi ya watu Ili kuepuka migogoro na  wananchi.

Kisha Mwenge wa Uhuru ukaelekea katika shule ya sekondari ya Tulindane katika kijiji cha Lingana ambako umezindua shule hiyo.

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Godfrey Mzava amesema ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kuongeza kuwa utakuwa mkombozi kwa wakazi wa Kijiji hicho.

Kituo kilichofuata baada ya uzinduzi huo ni kituo Cha Afya cha Zulu katika kijiji Cha Lichungu ambapo Mwenge wa Uhuru pia ulizindua mradi huo unaomilikiwa na mtu binafsi Ndg. Issa Lalikila.

Mhe. Mzava amempongeza mmiliki wa kituo hicho kwa ubunifu wake wa kuwekeza katika sekta ya Afya hatua ambayo amesema itasaidia kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za Afya katika Mji wa Newala.

Ukiwa katika kijiji hicho cha Lichungu Mwenge wa Uhuru umetembelea kuona na kukagua shughuli za wajasiliamali, vijana, Wanawake na wenye  ulemavu pamoja na kukabidhi madawati, viti na meza kwa shule za msingi na sekondari mradi wenye thamani ya shilingi Milioni 57.4.

Pia Mwenge wa Uhuru ulikagua na kuona mradi wa ujenzi wa Tanki la Maji lenye ujazo wa lita Milioni 6 katika kijiji cha Nambunga wenye thamani ya shilingi Bilioni 2.2.

Aidha kiongozi wa mbio za Mwenge  Mhe. Godfrey  Mzava alihitimisha ziara ya mbio za Mwenge  katika Halmashauri ya mji wa Newala kwa kuona na kukagua shughuli za Malaria, UKIMWI, na Lishe. Pia alikagua klabu ya kupambana na dawa za kulevya, rushes pamoja na banda la  kutoa elimu ya uchaguzi.

Mwenge wa Uhuru utaendelea kukimbizwa  Wilayani Newala hapo kesho ambapo itakuwa zamu ya Halmashauri ya Wilaya  ya Newala.


Juni 03, 2024


#TunaifunguaMtwara

#KaziInaendelea


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA.

    June 24, 2025
  • MKURUGENZI MPYA NANYAMBA NA DAS MPYA MTWARA WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

    June 23, 2025
  • MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA UTEGEMEZI KWA WAFADHILI.

    June 28, 2025
  • MAREKANI KUTUMIA BANDARI YA MTWARA KUSAFIRISHA BIDHAA

    June 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.