• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MBIO ZA MWENGE WA UHURU WILAYANI TANDAHIMBA MKOANI MTWARA

Posted on: June 2nd, 2024


Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 Mkoani Mtwara leo Juni 2 zimebisha hodi katika Wilaya ya Tandahimba.

Ukiwa Wilayani hapa Mwenge wa Uhuru umezindua Miradi, umeweka mawe ya msingi pia umetembelea na kuona Miradi 7 yenye thamani ya shilingi Bilioni 3.78.

Mara baada ya kuwasili Mwenge wa Uhuru ulielekea katika Kijiji cha Lembela Kata ya Mihambwe ambako ulikagua na kuona Miradi wa ufugaji kuku wenye thamani ya shilingi Milioni 33 unaolenga kuwawezesha vijana Kiuchumi.

Kisha Mwenge ulielekea katika Kata ya Kitama Kijiji Cha Kitama shuleni ambako uliweka jiwe la msingi katika Mradi wa Ujenzi wa Kituo Cha Afya Kitama Uliogharimu shilingi Milioni 469.

Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Ndg. Godfrey Mzava amewaambia mamia ya Wananchi waliojitokeza kuulaki Mwenge kuwa. Serikali imedhamiria  kuwasogezea wananchii huduma za Afya  huku akiitaka Halmashauri ya Wilaya ya  Tandahimba kukikamilisha kituo hicho  Ili kiweze kuwahudumia wananchi.

Kituo kilichofuata kulikuwa ni Tandahimba mjini ambako Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi Mradi wa Ujenzi wa barabara kiwango Cha lami wenye thamani ya shilingi Milioni 949.4.

Akizungumza katika eneo la Mradi huo Kiongozi wa mbio za Mwenge  Kitaifa Ndg. Godfrey Mzava amesema Serikali inatumika fedha nyingi kukamilisha miradi ya barabara huku akiwataka wananchi kuitunza ili idumu kwa muda mrefu.

Aidha  Mzava amepongeza wakala wa barabara vijijini TARURA kwa kukidhi vigezo vya taratibu za manunuzi katika matumizi ya mfumo wa NEST.

Mradi mwingine uliotembelewa  na Mwenge wa Uhuru mjini Tandahimba ni Mradi wa jengo la Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Mradi Uliogharimu kiasi Cha shilingi milioni 281.

Kisha Mwenge wa  Uhuru  ukaelekea Kijiji Cha Malamba Kata ya Malopokelo kukagua na kuona shughuli za upandaji miti na uhifadhi wa mazingira katika shamba la miti Malamba, Mradi uliogharimu shilingi Milioni 7.4.

Baadae ziara ya Mwenge wa Uhuru iliendelea katika Kata ya Mkundi katika Kijiji Cha Chitoholi A ambako Mwenge wa  Uhuru uliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji Chitoholi uliogharimu shilingi Bilioni 1.4.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Geoffrey Mzava amewaambia Wananchi waliofika kuulaki Mwenge kuwa Serikali kwa kutambua adha ya upatikanaji wa maji safi imeamua kuwekeza katika mradi huo na kuwataka wakazi wa Chitoholi na maeneo jirani kutunza miundombinu yake. 

Aidha amewapongeza Wakala wa Usambazaji Maji Safi Vijijini na Usafi wa Mazingira RUWASA kwa kutumia vigezo vya mfumo wa manunuzi wa NEST  ambao umeisaidia Serikali kuepuka hasara na vitendo vya ubadhilifu.

Mradi wa mwisho uliohitimisha ziara ya Mwenge wa Uhuru ni ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya Makondeni mradi uliogharimu shilingi Milioni 560.5.

Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Mtwara 2024 zitaendelea tena hapo kesho Wilayani Newala.


Juni 02, 2024


#TunaifunguaMtwara

#KaziIendelee


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA.

    June 24, 2025
  • MKURUGENZI MPYA NANYAMBA NA DAS MPYA MTWARA WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

    June 23, 2025
  • MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA UTEGEMEZI KWA WAFADHILI.

    June 28, 2025
  • MAREKANI KUTUMIA BANDARI YA MTWARA KUSAFIRISHA BIDHAA

    June 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.