• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MELI KUBWA YENYE MAKASHA YAPOKELEWA MKONI MTWARA

Posted on: October 22nd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bi Mwanahamisi Munkunda leo Oktoba 22, 2023 ameungana na viongozi wa Chama na serikali Mkoani Mtwara kupokea Meli Kubwa yenye makasha zaidi ya 225 katika bandari ya Mtwara yatakayotumika kusafirisha Korosho kuelekea Nchi mbalimbali duniani.


Mkuu wa huyo wa Wilaya ya Mtwara Bi Mwanahamisi  Munkunda amesema kuwa ujio wa meli hiyo ni utekelezaji wa agizo la Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Wakati wa ziara yake Mkoani Mtwara ambapo aliuagiza uongozi wa Mkoa kuhakikisha unaanza kuitumia bandari yake kusafirisha korosho Ili kupanua wigo wa soko la zao hilo.


Aidha Mhe Munkunda ametoa wito kwa wadau mbalimbali Mkoani Mtwara wakiwemo wafanyabiashara, wasafirishaji, wakulima, watoa huduma pamoja na wadau wote wanaoguswa na mnyororo wa thamani katika suala zima la Kilimo na usafirishaji wa Korosho kupitia bandari ya Mtwara kuchangamkia fursa hiyo Ili waweza kujikwamua kiuchumi.


" Ndugu viongozi mliopo hapa pamoja na Wanahabari, bila shaka wote mmeshuhudia mwisho ni mwa wiki tunayoimaliza Leo tulizindua mnada wa kwanza wa Korosho ambapo mpaka sasa tumeuza tani elfu 20" alisema Mhe Mwanahamisi Mnkunda.


" Hivyo ni matumaini yangu kuwa ujio wa meli hii utaleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi kwa wanamtwara wakiwemo mama ntilie, boda boda, bajaji, wamiliki wa Nyumba za kulala wageni halikadhalika wakulima na wanunuzi wa korosho kwa ujumla ninawaomba mchangamkie fursa" akisisitiza Mhe Munkunda.


Aidha Mkuu wa Wilaya Mhe Munkunda ameuagiza uongozi wa Bandari ya Mtwara kujiweka Mkakati wa kuwavutia wamiliki wa meli Kutoka maeneo mbalimbali duniani wasafirishe mzigo wa Korosho kupitia bandari hiyo.


Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Mtwara Frednand Nyathi amemhakikishia Mkuu huyo wa Wilaya kuwa tayari wamejipanga kuhakikisha mzigo wote wa Korosho utakaosafirishwa kupitia bandari hiyo unawafikia wateja kwa Wakati na kuongeza kuwa kutokana na uwepo wa miundombinu ya kisasa iliyopo kazi hiyo itatekelezwa kwa ufanisi.


Baadae mwezi ujao bandari ya Mtwara inatarajia kupokea zaidi ya meli 7 Kutoka Nchi mbalimbali zitakazofika kuchukua shehena ya Korosho.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.