Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala Leo juni 11, 2025 ametembelea na kukagua miradi ya maendeleo ya sekta ya Elimu Katika halmashauri ya wilaya Masasi , Nanyumbu na Mji Masasi.
Siku ya pili ya ziara yake Katika halmashauri ya wilaya Masasi, amekagua mradi wa shule ya msingi ya Mkondo Mmoja katika kijiji cha Mkwaya Mradi uliotekelezwa Kwa gharama milioni 334.6.
Akizungumza na wakazi wa kijiji hicho mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa shule hiyo Kanali Sawala amewaeleza Wananchi kuwa serikali imedhamiria kuboresha mazingira ya utoaji elimu nchini Ili kuhakikisha idadi kubwa ya Watoto wanapata nafasi ya kusoma
"Ndugu wananchi mmekua mashahidi jinsi serikali yenu inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyowajali, mbele yenu huu ndio ushuhuda, Sasa Miundombinu yote Iko tayari pelekeni watoto shuleni, pili hakikisheni wanapata chakula bila kusahau kuzingatia malezi bora yanayoendana na mila na desturi za mtanzania" alisema Kanali Sawala
Sambamba na mradi wa ujenzi wa shule ya msingi Mkondo Mmoja Mhe. Kanali Sawala amekagua mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Mnavira ,shule ya sekondari Amali Mbuyuni, shule mpya ya ufundi Masasi shule ya sekondari Matawale pamoja na shule ya sekondari Kilimanihewa yenye thamani ya zaidi ya billion 4.1
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara
Anuani ya Posta: 544, MTWARA
Simu: +255 23 2333014
Mobile: +255 23 2333014
Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz
Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.