• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Majaliwa awataka Watumishi wa Umma kutekeleza wajibu wao

Posted on: February 27th, 2018

Baadhi ya mabango yaliyowasilishwa kwa Mheshimiwa Majaliwa katika Mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Newala


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa amewataka watumishi wa Umma kote nchinI kuhakikisha wanawatumikia wananchi katika misingi ya haki na maadili ya kiutumishi. Amesema huo ndio utumishi wa umma unaosisitizwa na serikalini ya awamu ya Tano na kwamba yeyote atakayeshindwa kutekeleza hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

 Mheshimiwa Majaliwa ambaye yuko katika siku ya pili ya ziara ya Kikazi Mkoani Hapa ameyasema hayo leo katika kikao na Watumishi wa Halmashauri za Wilaya na Mji wa Newala kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Amesema taratibu za serikali zinaeleweka ambapo kila mtumishi wa Umma ana sehemu yake ya utekelezaji wa majukumu yake ya kazi ikiwemo kuwahudumia wananchi. Inapotokea nidhamu ikakosekana, ushirikiano hupotea na hatimaye kupoteza ufanisi wa kazi.

Ameongeza kuwa Kila Mtumishi wa Umma anapaswa kuijua ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo inatekelezwa. Hilo litamsaidia Mtumishi kufahamu nini anachotakiwa kufanya kwani watanzania walikiamini chama cha Mapinduzi na kukipa nafasi ya kuongoza nchi, kwa maana hilo kila mtumishi bila kujali imani yake au itikadi yake kisiasa anapaswa kuhakikisha anashiriki katika kuitekeleza ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Awali akiwasilisha taarifa ya Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Newala Mheshimiwa Aziza Mangosongo amesema Halmashauri zote mbili za Wilaya ya Newala zimejipanga kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo katika wilaya kwa weledi. Amesema ziko changamoto nyingi katika utekelezaji wa majukumu hayo lakini wamejipanga kupambana nazo. Amezitaja baadhi ya changamoto kuwa ni pamoja na miundombnu chakavu ya utoaji wa huduma ikiwemo matatizo umeme, barabara na Maji.

Nakuhakikishai Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba wananchi wa Newala wako tayari kuhakikisha ilani ya Chama inatekelezwa kama Serikali ya awamu ya tano ilivyoelekeza.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa yuko katika ziara ya siku tatu Mkoani Mtwara. Katika Siku hizo tatu ambazo zitakamilika kesho Februali 28, Mheshimiwa Majaliwa atapita Wilaya zote tamo za Mkoa wa Mtwara akifanya vikao na kukagua miradi mbalimbali ya Mendeleleo

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.