• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Mkuchika alia na elimu Mtwara.

Posted on: January 2nd, 2018


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu Mhe. George Huruma Mkuchika amewataka wananchi wa Mtwara kuchangamukia Elimu.

Mheshimiwa Mkuchika ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Newala Mjini ameyasema hayo akiwa katika kijiji cha Lwelu kilicho Manispaa ya Mtwara Mikindani ambako alikuwa akikagua miradi inayotekelezwa kupitia mpango wa TASAF.

Akitumia maandiko matakatifu Mheshimiwa Mkuchika amesema hata Kitabu cha Mithali ndani ya Biblia Takatifu kinawataka wakristo kuishika sana Elimu na wasiiache, halikadhalika Quran Takatifu inawataka waislam kuitafuta sana elimu hata kama ni kwa kuifuata nje ya Nchi.

Amesema yeye kama mzaliwa na Mtwara na Mbunge wa jimbo ndani ya Mkoa wa Mtwara haridhishwi na hali ya eilimu mkoani Mtwara. Amesema mkoa umekuwa ukishika nafasi za mwisho katika mitihani ya Taifa kutokana na wananchi wa mkoa wa Mtwara kutoweka jitihada kubwa katika elimu.

Amewataka wazazi kuhakikisha watoto wanafanya vizuri katika mitihani kwa kutimiza wajibu wao. Ametaja moja ya majukumu makubwa ya wazazi kuwa ni pamoja na kuchangia mambo mbalimbali ya kielimu ikiwemo kuwawezesha watoto kupata huduma ya chakula.

‘Nimekuja kufuatilia mambo ya TASAF lakini lazima niliseme hili kwani TASAF inatoa misaada mbalibmali ya kuwawezesha watoto kwenda shule lakini wazazi wana nafasi ya kuhakikisha malengo yaliyokusudiwa katika mpango yanafikiwa huku na wao wakifanya jitihada zao binafsi kuhakikisha watoto wanapata elimu’. Alisema Mkuchika

Awali wakiwasilisha taarifa ya hali ya maendeleo ya utekelezaji wa Miradi ya TASAF wananchi wa kijiji hicho walielezea changamoto ya Elimu ambapo vipo vijiji ambavyo vinasafari umbali mrefu kuifuata elimu na hivyo kumtaka waziri asaidie kutatua changamoto hiyo.

Akifafanua suala hilo Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmand amesema anatambua changamoto hiyo na kuahidi kuifanyia kazi.

Mkoa wa Mtwara Umekuwa haufanyi vizuri katika mitihani ya Kitaifa ambapo matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Pili 2017 mkoa ulitoa shule 9 za mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.