• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MTWARA TUNATHAMINI KAZI KUBWA INAYOFANYWA NA MHE. RAIS YA KUINUA SEKTA YA MICHEZO - KANALI AHMED ABBAS AHMED.

Posted on: February 22nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed leo amefika katika Ofisi za GSM jijini Dar es Salaam kutimiza ahadi yake ya kuziunga mkono timu za Simba Sc na Yanga Sc zinazoshiriki mashindano ya Kimataifa.

Mapema wiki iliyopitaKanali Abbas aliahidi kutoa kiasi cha shilingi 1000,000/= kwa kila goli litakalofungwa na timu za YangaSc na Simba Sc zinazoshiriki mashindano ya Kimataifa ambapo Jumapili iliyopita Februari 19 Yanga Sc iliifunga TP Mazembe magoli 3 - 0.

Akikabidhi kitita cha shilingi 3,000,000/= kwa Rais wa Yanga Eng. Hersi Said kutimiza ahadi yake, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema wanamtwara wote wanatambua na kuthamini kazi nzuri ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye usiku na mchana amekuwa mstari wa mbele kuziunga mkono sekta mbalimbali ikiwemo michezo na kuongeza kuwa ametoa motisha hiyo kama ishara ya kuunga mkono jitihada hizo.

"Sote tunatambua Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan anafanya kazi kubwa kuhakikisha sekta zote ikiwemo michezo zinafanya vizuri, ndio maana sisi Mtwara tumeona tujitokeze kuunga mkono jitihada hizo tukiamini hatua hii itaongeza hamasa katika sekta ya michezo nchini" alisema Kanali Ahmed Abbas Ahmed.

Pia Kanali Abbas amemuomba Rais wa Yanga kuangalia uwezekano wa kuimarisha ushirikiano kati ya Klabu ya Yanga na Mkoa wa Mtwara ili kuinua sekta ya michezo sambamba na kuinua vipaji vipya.

Kwa upande wake Rais wa Club ya Yanga Eng. Hersi Said, baada ya kupokea motisha hiyo ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Mtwara kwa ubunifu huo na kuongeza kuwa Utamaduni huo utaongeza chachu ya ushindani miongoni mwa vilabu huku akiwataka wadau wengine wa soka kuiga mfano huo.

"Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza sana wewe Mhe. Mkuu wa Mkoa pamoja na timu yako kwa kuthamini mafanikio ya timu yetu ambayo juzi imepeperusha vema bendera yaTaifa " alisema Eng. Hersi.

Halikadhalika Eng. Hersi Said amemuahidi Mkuu wa Mkoa kuwa, club ya Yanga iko tayari kushirikiana na Mkoa wa Mtwara ambao ameutaja kuwa miongoni mwa maeneo yenye fursa nyingi za kiuchumi.

Eng. Hersi ameongeza kuwa kwa muda wa wiki moja kuanzia leo mitandao yote ya kijamii ya club ya Yanga itarusha habari zinazoutangaza Mkoa kama njia ya kudumisha ushirikiano.

Aidha Mkuu wa Mkoa Kanali Ahmed Abbas Ahmed amemuomba Eng. Hersi Said kupitia vyombo vya habari vya Yanga kuwahabarisha wananchi kuhusu shughuli ya Uzinduzi wa Mwenge wa Uhuru utakaozinduliwa katika Uwanja wa Nangwanda Aprili 2 mwaka huu.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA.

    June 24, 2025
  • MKURUGENZI MPYA NANYAMBA NA DAS MPYA MTWARA WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

    June 23, 2025
  • MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA UTEGEMEZI KWA WAFADHILI.

    June 28, 2025
  • MAREKANI KUTUMIA BANDARI YA MTWARA KUSAFIRISHA BIDHAA

    June 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.